Recent Posts

PropellerAds

Friday, July 28, 2017

Zawadi kuu



Image result for greatest gift of all 
Na kenedy Jagaji
Upendo wa MUNGU kwa mwanadamu hauna mwanzo wala mwisho, MUNGU hupenda siku zote na yupo tayari kukupokea endapo utamkiri na kumfuata
Yakobo 4:8
“mkaribieni MUNGU,naye atawakaribia ninyi”
Na  sisi tumeona na kushuhudia yakuwa Baba amemtuma mwana kua mwokokozi wa ulimwengu,  na sisi tumelifahamu pendo alilo nalo kwetu sisi na kuliamini Mungu ni pendo , naye akaaye katika pendo hukaa ndani yake.
1 yohana 6:14,16

Biblia inatukumbusha kuhusu Baraka na ahadi ambazo Mungu atupazo kila siku , jambo muhimu la kuzungumzia ni  kuhusu  jinsi gani Mungu anatupenda hata kumtoa mwanae kwa kile ambacho alikiumba kwa mkono wake kisipotee. Hii ni moja ya kazi kubwa na sadaka ya pekee katika ulimwengu ambayo haitatokea daima na ni upendo usio na kifani katika kazi ya Mungu kwa Mwandamu.
Sasa ni wakati wako wa kumshukuru Mungu kwa zawadi yake ya pekee kwako na utambue upendo  mkuu wa Mungu katika maisha yako ya kila siku kuna kitu ambacho ni zaidi ya kazi yako, familia yako pesa na utajiri wako . jambo ambalo Mungu anahitaji kutoka kwako ni shukrana na kuwapenda wengine kama alivyo kupenda wewe.
Kristo analikufa  kwa ajili yako.
Hapa tunaweza kufikiri kuhusu upendo wa yesu kristo kwako, yesu anakupenda sana hata kuutoa uhai wake kwa ajili yako, tena uiishi milele.
Je ni nani anaeweza kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake? Jibu ni hapana  kwa wanadamu
“kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwae wa pekee ili kila mtu amwaminie asipotee, bali awe na uzima wa milele maana Mungu hakumtuma  mMwana ulimwengununi ili ahukumu aulimwengu  bali ulimwengu uokolewe katika yeye”

Yohana 3:16
Kifo ni ishara ya mwanzo mpya wa maisha  mengine.
Hakuna hata mmoja ajuae lini na wapi atakufa lakini hutokea kwa kila mmoja , lakini kifo ni jambo ambalo kila mtu anahitaji kujiaanda nalo. Kwanini? Kwa sababu kifo ni sehemu ya maisha ya mwandamu . unapopanga mipango yako ya maisha kumbuka kupanga pia kuhusu maisha yako baadaa ya kufa . ni vema uwe tayari kuishi na kufa kuanzia  sasa.