Recent Posts

PropellerAds

Thursday, July 21, 2016

Utafiti: Harufu ya kuku inazuia Malaria

Je unaogopa kuambukizwa na ugonjwa wa malaria ?
Ikiwa jibu lako ni ndio basi nakupa ushauri nasaha,,
Fuga kuku !
Utafiti umebaini kuwa ,harufu ya kuku inaweza
kukulinda dhidi ya maambukizi ya malaria.
Watafiti nchini Ethiopia na Sweden wamegundua kuwa
mbu wanaobeba vimelea visababishavyo ugonjwa wa
Malaria huwa wanafanya kila wawezalo kukaa mbali na
ndege huyo anayefugwa majumbani.
Moja kati ya majaribio katika utafiti huo ilijumuisha
kumweka kuku aliyehai karibu na mtu aliyelala chini ya
chandarua kinachozuia kuumwa na mbu.
Mwaka uliopita watu laki nne 400,000 walikufa kutokana
na ugonjwa wa malaria barani Afrika, kwa mujibu wa
takwimu za Umoja wa Mataifa.
Japo idadi na visa vya maambukizi ya Malaria
vinaendelea kushuka, wataalamu wanaendelea kutafuta
mbinu bora zaidi ya kuangamiza kabisa ugonjwa huo.
Vimelea vya malaria hujificha ndani ya maini kabla ya
kuambukizwa kutoka kwa mwanadamu mmoja hadi
mwengine kupitia kwa mbu wa kike anayefyonza damu.
Utafiti huo uliochapishwa katika jarida la Malaria
umebaini kuwa mbu hunusa harfu ya mnyama kabla ya
kumuuma.
Hata hivyo hawajui nini katika harufu ya kuku inawapa
kinyaa mbu .
Katika hatua ya pili ya utafiti huo sasa, watafiti hao
wanalenga viungo vya harufu ya kuku ilikuunda kinga
dhabiti dhidi ya mbu hao wanaoambukiza malaria.
Habtie Tekie kutoka chuo kikuu cha Addis Ababa
Ethiopia anasema kuwa mipango inaendelea na huenda
majaribio yakatekelezwa karibuni.
Watafiti kutoka chuo kikuu cha kilimo cha Sweden
walihusika katika utafiti huu.
Iligundulika kuwa idadi ya mbu ilipungua kwa asilimia
kubwa sana mahala popote ambapo viungo vya kuku
vilitumika ima ni manyoya ama sehemu zingine za kuku.
Wanasayansi wanasema kuwa kuna haja ya kuendelea
kutafuta mbinu mpya za kukabiliana na mbu kwani hata
sasa mbu wanaonesha dalili ya kuwa sugu dhidi ya
madawa yaliyoko sasa.

Saturday, July 16, 2016

speak truth

The day we see the truth and cease to speak is the day we begin to die - Martin Luther King Jr.

great liabilities

One of the great liabilities of history is that all too many people fail to remain awake through great periods of social change. Every society has its protectors of status quo and its fraternities of the indifferent who are notorious for sleeping through revolutions. Today, our very survival depends on our ability to stay awake, to adjust to new ideas, to remain vigilant and to face the challenge of change. - Martin Luther King Jr.

another way to defeat your enemy

Another way that you love your enemy is this: When the opportunity presents itself for you to defeat your enemy, that is the time which you must not do it. There will come a time, in many instances, when the person who hates you most, the person who has misused you most, the person who has gossiped about you most, the person who has spread false rumors about you most, there will come a time when you will have an opportunity to defeat that person. It might be in terms of a recommendation for a job; it might be in terms of helping that person to make some move in life. That’s the time you must do it. That is the meaning of love. In the final analysis, love is not this sentimental something that we talk about. It’s not merely an emotional something. Love is creative, understanding goodwill for all men. It is the refusal to defeat any individual. When you rise to the level of love, of its great beauty and power, you seek only to defeat evil systems. Individuals who happen to be caught up in that system, you love, but you seek to defeat the system. - Martin Luther King Jr.

Thursday, July 14, 2016

Boris Johnson alivyokejeli Afrika na watu mashuhuri

Waziri mkuu mpya wa Uingereza Theresa May, amemteua Boris Johnson, aliyeongoza kampeni ya taifa hilo kujitoa katika Muungano wa Ulaya kuwa waziri wa mambo ya nje.
Johnson, ambaye aliwahi kuwa Meya wa jiji la London amesema Uingereza sasa ina nafasi kubwa kujenga upya uhusiano wake na Ulaya na ulimwengu mzima lakini ni ulimwengu ambao ameuuudhi kwa namna moja au nyengine kutokana na matamshi yake ya kejeli.
Haya ni baadhi ya maneno ya kejeli aliyoyatamka kuhusu:
Afrika
Mwaka 2002 wakati Waziri Mkuu wa zamani Tony Blair alipofunga safari ya kuzura bara Afrika Boris alisema; 'Ah ni lazima Blair anahisi afueni kuu kwamba hatimae amepata fursa ya kutoka Uingereza. Inasemekana Malkia siku hizi anapendelea sana maswala ya Jumuiya ya Madola, moja wapo ya sababu ni kuwa inampa fursa za mara kwa mara kuona tu umati wa watu wazima kwa watoto wanaomshangilia wakimpeperushia vibendera.!'
Kisha Boris akaongeza kusema '' Na baadayee ataelekea Congo. Sina shaka hizo AK47 itabidi zinyamaze, mapanga yanayotumiwa na waafrika kukatanakatana yatasitishwa kwa muda na wapiganaji wao wakikabila watatoa tabasamu za kama tikitimaji pindi wakimuona chifu mkuu Wakizungu Blair akitua na akiteremka kutoka ndege yake kubwa iliyonunuliwa na watoa kodi wa Uingereza.''
Japo Bw Johnson aliomba radhi kwa matamshi hayo mwaka 2008, alipopata cheo cha meya wa mji wa London, kauli hiyo haijasahaulika.
Kumhusu Obama
Na si hayo tu Machi mwaka huu wakati maafisa wa Marekani wanaohusika na maswala ya offisi ya Rais Barack Obama alipoamua kuiondoa picha ya Winston Churchill kutoka ofisi yake ya Oval , Boris alisema- ''Hakuna uhakika iwapo Obama mwenyewe alihusika katika uamuzi huo wa kuiondoa picha ya Churchill. Baadhi ya watu wanasema ni kwasababu kwa vile yeye ni nusu mkenya alichukizwa na kumbukumbu ya picha ya Winston ambaye aliunga mkono kwa dhati utawala wa Uingereza ulioikalia Kenya kwa mabavu enzi za ukoloni."
Kuhusu Uturuki
Kama Obama alihisi kuchokozwa Basi rais wa Uturuki ndio zaidi.
Utakumbuka mapema mwaka huu wakati Ujerumani ilipomshtaki raia wake mmmoja mchekeshaji aliyetunga shairi lililomdhalilisha rais Recep Tayyip Erdogan, gazeti moja la Uingereza litwalo The Spectator likaongezea maudhi hayo kwa kuandaa shindano la nani anaweza kutunga shairi la kumdhalilisha Erdogan zaidi ya hilo lililotungwa na mjerumani- Si tu kwamba Boris alishiriki shindano hilo bali pia aliibuka mshindi!
Kumuita Assad dikteta
Kuhusu uhusiano wa serikali ya Syria na Urusi - Baada ya majeshi yao kukomboa mji wa hifadhi za kumbukumbu za kale Palmyra
Boris alinukuliwa kusema 'mtu yoyote mwenye akili timamu anapaswa kufurahi kwamba Palmyra imekombolewa na majeshi ya Assad lakini wakati huohuo asibadili msimamo kwamba Assad ni Dikteta na Zimwi'
Kumshutumu Putin
Kisha akamshtumu Putin akisema operesheni zake za kijeshi zimekuwa zikilenga hospitali na shule za Syria lakini wakati huohuo akamsifu Putin na utawala wake huko Urusi.
Hapo May alihoji sera ya EU huko Ukraine ambako Urusi inashutumiwa kuwaunga mkono waasi wa mashariki wa Ukrain lakini Boris akasisitiza kuwa ni mfano wa
maamuzi ya EU yaliyofeli kutatua mzozo huo unaendelea hadi leo.
Msemaji wa serikali ya Urusi Dmitry Peskov amesema anatumai uteuzi wa Boris kama waziri wa mambo ya nje unatoa fursa ya mwanzo mpya baina ya mataifa hayo akiongeza kusema kuwa anatumai nafasi hiyo itamfanya Boris kuwa na msimamo mpya wenye mwelekeo wa kidiplomasia.
Tukitazama tena Marekani, Je Boris anasemaje kuhusu wagombea urais wa nchi hiyo ambao itabidi kukabiliana nao baada ya Novemba ambapo mmoja wao anatarajiwa kumrithi Obama?
Clinton na ‘nywele zilizopakwa rangi’
Mwaka 2007 hivi ndivyo Boris alivomwelezea Bi Hillary Clinton- 'ana nywele zilizopakwa rangi, midomo yake ilivyo na anavyokodoa yale macho yake ya blue, utafikiri ni nesi mwenye roho mbaya ndani ya hospitali ya watu wenye matatizo ya kiakili'
Boris anampenda Trump?
Kwa hivyo ni kusema kuwa Boris anampendelea Donald Trump?
La, hebu msikie alivyosema hapo mwezi Machi '' Kwa kweli nna wasiwasi mkubwa kwamba Trump anaweza kushinda! Na siku moja nilikuwa New York, wapiga picha walikuwa wanataka kunipiga picha karibu na mtoto mmoja - mtoto yule akanisogelea kisha akauliza 'Gee, kwani huyu ni Trump?'
Nilijisikia vibaya sana!' Itakumbukwa Boris amekuwa akimtaja Trump kuwa 'mtu asiyejua akisemacho kama vile hana akili nzuri'.
Na kejeli hizo anajulikana kuziendeleza tangu akiwa Meya wa London.
Boris Johnson amewahi kuwaudhi pia baadhi ya mataifa ya Uarabuni na hata Papua New Guinea ambao hawajaupokelea vyema uteuzi wake.

Ndege ya kisasa ya Ethiopia yatua Kenya

Ethiopia imekuwa taifa la kwanza barani Afrika
kununua ndege ya kisasa aina ya Airbus A350 XWB.
Ndege hiyo, Airbus A350, ndiyo ya hivi karibuni
kuzinduliwa na kampuni ya ndege ya Airbus ya
Ufaransa.
Ndege hiyo, iliyo na uwezo wa kubeba zaidi ya abiria
300, ilitua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa
Jomo Kenyatta jijini Nairobi Kenya Jumatano jioni
ikitokea mjini Addis Ababa, Ethiopia.
"Ndege hii ya kisasa itasaidia katika utoaji wa huduma
zetu, kuimarisha mtandao wetu wa usafiri, na
kupunguza kwa kiasi kikubwa viwango vya hewa chafu
inayotolewa wakati wa usafiri wa ndege,” Mkurugenzi
mkuu wa shirika la Ethiopian Airlines Tewolde
GebreMariam amesema.
Ndege hiyo ni ya kwanza kuwasilishwa kwa kampuni
hiyo, huku nyingine 13 ilizoagiza kutoka kwa kampuni
ya Airbus zikisubiriwa hivi karibuni.
Safari ya kwanza ya ndege hiyo ilifanyika tarehe 2 Julai
iliposafiri kutoka Ufaransa hadi mjini Lagos, Nigeria.
Viwango vya juu vya teknolojia iliyotumika kuunda
ndege hiyo, vinachangia katika kuinua utendakazi wake,
kupunguza matumizi ya mafuta pamoja na kupunguza
kwa kiasi kikubwa utoaji wa hewa chafu.
Ndege isiyotumia mafuta yatua Misri
Ndege kubwa zaidi duniani yatua Australia
Kampuni ya Ethiopian Airlines inaorodheshwa ya
kwanza barani Afrika kwa faida na pia idadi ya maeneo
inayosafirisha abiria.
Mwaka wa 2012, shirika hilo pia lilikuwa la pili duniani
na la kwanza barani afrika kununua ndege aina ya
Boeing 787 Dreamliner, ya kampuni ya Boeing, yenye
afisi zake kuu Chicago, Marekani.
Kampuni ya Airbus na Boeing zinaongoza duniani katika
utengenezaji wa ndege za kisasa, japo Airbus ina
umaarufu mkubwa na imeipiku Boeing kwa faida na
uuzaji wa idadi kubwa ya ndege.

Tuesday, July 12, 2016

Malala asherehekea siku ya kuzaliwa Kenya

Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel Malala Yousafzai
amezuru kambi ya wakimbizi ya Dadaab kaskazini
mashariki mwa Kenya ambapo atasherehekea siku
yake ya kuzaliwa.
Malala alizaliwa 12 Julai 1997 eneo la Mingora,
Pakistan katika bonde la Swat.
Alihudhuria shule iliyoanzishwa na babake Ziauddin
Yousafzai na baada ya wanamgambo wa Taliban
kuanza kushambulia shule za wasichana Swat, alitoa
hotuba Peshawar, Pakistan akishutumu Taliban kwa
kumnyima wasichana haki ya msingi.
Akiwa na umri wa miaka 14, yeye na familia wake
walifahamu kwamba Taliban walikuwa wametoa vitisho
kwamba wangemuua.
Tarehe 9 Oktoba, 2012, akirejea nyumbani kutoka
shuleni, akiwa kwenye basi, mtu mwenye silaha
alimpiga risasi kichwani.
Malala ashinda tuzo ya amani ya Nobel
Alipelekwa Birmingham, Uingereza ambapo alipokea
matibabu na Machi 2013 akaanza kwenda shuleni.
Mwaka huo pia, aliandika kitabu kuhusu maisha yake.
Aliteuliwa kushindania tuzo ya amani ya Nobel 2013
lakini hakushinda. Aliteuliwa tena 2014 na akashinda
kwa pamoja na mwanaharakati mwingine Kailash
Satyarthi.
Alikuwa na umri wa miaka 17 na ndiye mtu wa umri
mdogo zaidi kuwahi kushinda tuzo hiyo.
Amekuwa akitetea haki za watoto na wanawake.

Moise Katumbi: Serikali ya DRC ilijaribu kuniua

Kiongozi wa upinzani nchini DRC ambaye pia ni
mgombea wa kiti cha urais katika uchaguzi ujao
amesema kuwa serikali ya rais Joseph kabila ilimpa
sumu katika njama ya kumuua.
Mwanasiasa Moise Katumbi wa Jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo anasema kuwa alidungwa
sindano iliyokuwa na sumu nje ya mahakama ya
Lubumbashi mnamo mwezi Mei.
Katumbi anasema haikujulikana sindano hiyo ilikuwa na
nini.
Hata hivyo anasema askari polisi mmoja alimdunga
sindano katika mshikemshike nje ya mahakama polisi
walipofyatua mabomu ya kutoa machozi kwa mashabiki
wake alipokuwa akienda kujibu mashtaka ya kuwaajiri
mamluki kuwa walinzi wake kinyume cha sheria.
Bw Katumbi anasema kuwa madai hayo dhidi yake ni
ya ''upuuzi''.
Hata hivyo kiongozi huyo ambaye ni mkurugenzi mkuu
wa klabu ya TP Mazembe aligonjeka na akalazimika
kukimbilia nje ya nchi ilikupata matibabu.
Katumbi ameiambia shirika la habari la AFP kuwa
alikwenda Afrika Kusini Uingereza na kisha Ujerumani
kutafuta tiba.
Waziri wa mawasiliano bwana Lambert Mende hakujibu
mawasiliano dhidi ya serikali yake lakini kwa siku nyingi
amepuuzilia mbali tuhuma kuwa polisi wa DRC
walimdhuru bwana Katumbi.

Saturday, July 9, 2016

"Everybody has a wheelchair"

Bert Burns understands God has a plan for our lives

By Duane Cross
We are hard pressed on every side, but not crushed; perplexed, but not in despair; persecuted, but not abandoned; struck down, but not destroyed. — 2 Corinthians 4:8-9

ALPHARETTA, Ga. — Listening to Bert Burns, you cannot avoid feeling ... uplifted. It's strange. It's hard to put into words. It's even more difficult when reality sets in: This dude is in a wheelchair — and he's having a better day than most of the people I know, including me.

It wasn't always this way, confined to a two-wheel horse, powered by Olympic medal-winning arms. Bert was not born with physical issues. He was an athlete growing up. He had dreams like many others. But dreams and real life don't always fit hand-in-glove.

Sometimes, it's even better ...

The paramedics said, 'Yeah, go clean that guy up; he's dead.'
— Bert Burns
It always seems to happen this way: A normal day in the life, driving along, minding the rules of the road. A hospital stint and rehab are the last things on your mind. I mean, you haven't reached the quarter pole in life; everything is ahead of you. Life is just there, ready to be lived. ... It was one of those days for Bert.

While driving home from work, that was Bert's reality. Seconds later, a drunk driver ran a red light, and the impact ejected Bert from his vehicle.

Life as he knew it was changed. Even the initial first responders had given up on Bert. When two other paramedics arrived at the scene they were tasked with cleaning up the 'dead' guy. ... But the guy wasn't dead. The reality was that Bert suffered a broken neck at the C6 and C7 vertebrae, and in the blink of an eye became a quadriplegic.

In fact, Bert Burns still had a lot of living to do. He still had a sales job to take. He still had to meet the love of his life. He had kids to raise. He had presidents, plural, to meet. He had a business to build. Bert still had life.

Bert still had his infectious personality to share with the world, most notably with Joy, his wife, and their children, twins Will and Emma.

The couple met on a sales call in Kansas. Listening to Bert tell the story, Joy was smitten before she knew it. They were married, in his head, during their first date. (They formally married in 1995.) As Bert recalls meeting Joy, you understand what she means to him, the love that Bert has shines through his eyes as they dance while remembering their first encounter.

Again, you wonder how this guy is so ... happy. You realize, he's not bound by the wheelchair. More than 30 years ago, Bert came to terms with his injury. His spine was broken — not his spirit.


Image result for wheelchair


Bert also is a gold medal cyclist. Yes, 10 years after his life changed forever, Bert was on the U.S. team that was atop the medal stand after the 4x400 relay during the 1992 Summer Paralympics in Barcelona, Spain. The U.S. topped the medal count with more gold (75), silver (52), and overall medals (175).

Ten years. I cannot fathom wanting to do much more than suck down a SunDrop and munch on Cheetos in the wake of being confined to a wheelchair, even 10 years later. ... And yet, listening to Bert, feeling sorry for himself and being overcome by what could have been was not an option.

Our first meeting with Bert was a lunch arranged by a mutual friend, Hal White. As Jacob Harkey, our video production lead, and I entered the restaurant, we immediately saw Hal and made our way to the table. Jacob sat across from me, with Bert to my right. I never noticed the wheelchair. Two months later, I wonder if that's a good thing, or if subconsciously I knew it had to be there and chose not to pay attention.

This is what I do know: Bert Burns chose to make a difference in others' lives. Life After Spinal Cord Injury is his ongoing work. He has speaking engagements. He enjoys vacations — cruises, skiing, scuba diving. "Everybody has a wheelchair," he says, but it does not confine or define Bert.

Bert is well respected in healthcare, too. He founded UroMed, an industry-leading catheter supply company. After all, who better to know how to assist those with challenges than someone who lives it? ... And there it is again — Bert being Bert, helping others, overcoming, surpassing expectations.

This story is not about "Oh, poor Bert Burns ... he's in a wheelchair." This story is about Bert Burns, who is not crushed, in despair, abandoned, nor destroyed.

Mamia kupigwa picha za utupu Uingereza

Tunick
Mamia ya watu watavua nguo zao na kupigwa picha wakiwa tupu kusherehekea utamaduni katika mji wa Hull, Uingereza.
Tukio hilo litakuwa la kusherehekea mji huo kama Mji wa Utamaduni.
Washiriki watapakwa rangi ya samawati Jumamosi na kisha wapigwe picha wakiwa katika maeneo mashuhuri jijini humo kama sehemu ya mradi uliopewa jina Sea of Hull.
Mradi huo unatekelezwa na mpiga picha Spencer Tunick na unadhaminiwa na taasisi ya Sanaa ya Ferens Art Gallery.
Picha zitakazopigwa zitawekwa na kuoneshwa kwa umma wakati wa tamasha ya sanaa ya 2017 itakayoendelea kwa mwaka mmoja.
Tunick, anayetoka New York, amewahi kufanya kazi kama hiyo kwingine.
Amewahi kupiga picha za watu wengi wakiwa uchi Sydney Opera House, Place des Arts mjini Montreal, Mexico City na mjini Munich nchini Ujerumani Germany.
Bw Tunick amesema kazi zake “hugusia historia ndefu ya Sanaa ya utupu”.
"Mavazi ni Sanaa ya mtu mwingine,” anasema.
“Fashoni ni Sanaa. Kwa kuondoa hilo (mavazi), nitakuwa nafanya kazi na usawa na maumbile katika umaridadi wake.”

Korea Kaskazini yarusha kombora jingine


Maafisa wa kijeshi nchini Korea Kusini wanasema Korea Kaskazini imejaribu kurusha kombora kutoka kwa manowari ya kivita na kukiuka vikwazo vya kimataifa
Wanasema kuwa kombora hilo hatahivyo lilifeli muda mfupi baada ya kurushwa
Urushaji huo wa kombora unajiri baada ya Korea Kusini na Marekani kukubaliana kuweka mitambo ya kujikinga dhidi ya makombora nchini Korea Kusini.

Mitambo hiyo ina uwezo wa kutambua makombora na kisha kuyadungua.
Nchi hizo mbili ziliafikia mpango huo baada ya majaribio kadha ya makombora yaliyofanywa na Korea Kaskazini mapema mwaka huu.

Sudan Kusini:Idadi ya waliouawa haijulikani


Ripoti kutoka mji mkuu wa Sudan Kusini Juba ,zinasema kuwa mili mingi imepelekwa katika hospitali kuu ya mji huo baada ya ufyatulianaji mkali wa risasi kuibuka karibu na nyumba ya rais siku ya Ijumaa.
Idadi ya watu waliouawa hatahivyo haijulikani.
Ufyatulianaji huo ulianza wakati ambapo rais Salva Kiir na makamu wake Riek Machar walikuwa wakijadiliana kuhusu ghasia siku ya Alhamisi baada ya wanajeshi watano wa serikali kuuawa katika vita vya pande pinzani.

Viongozi wote wawili wametaka kuwepo kwa utulivu.
Ghasia hizo ni mbaya zaidi kuwahi kutokea tangu makamu wa rais Riek Machar kurudi mjini Juba mnamo mwezi Aprili na vilevile zinajri wakati ambapo taifa hilo changa zaidi duniani liko katika harakati za kuadhimisha mwaka wa tano tangu lijipatie uhuru wake.

Wednesday, July 6, 2016

Mtandao unaowaunganisha wapenzi wa Kiislamu wadukuliwa


Maelezo ya kibinafsi ya takriban wanachama 150,000 wa mtandao unaowaunganisha wapenzi wa Kiislamu umewekwa wazi mtandaoni.
Zaidi ya ujumbe 700,000 za kibinafsi kati ya wanachama zimefichuliwa.
Ujumbe katika mtandao huo ulisema: ''Tumejulishwa kuhusu udukuzi na tunaurekebisha mtandao wetu kwa lengo la kuimarisha usalama wake''.
Ujumbe uliofichuliwa ulihusisha habari za siri kama vile iwapo mwanachama angependa kuwa na wake wengi.
Udukuzi huo ulibainiwa na mtafiti wa maswala ya kiusalama Troy Hunt ambaye anamiliki mtandao wa maswala ya usalama wa mitandaoni.

Maelezo kuhusu waajiri wa wanachama,akaunti zao za Skype na anwani zao za kuingia mtandao kulingana na mtandao wa teknolojia Motherboar.
Ukurusa wa kuwaunganisha waislamu wapendanao katika facebook ulielezea mtandao huo kuwa :Wasio katika ndoa,waliotalakiana,walio katika ndoa,''Ujumbe mmoja uliofichuliwa ulisema: Nataka kukuoa-iwapo unakubali nikutumie picha na maelezo yangu''.

Mamba anayebashiri matokeo ya uchaguzi Australia


Gazeti moja nchini Australia limedai kwamba kuna mamaba anayeweza kubashiri matokeo ya uchaguzi nchini Australia.
Gazeti hilo la Northern Territory News ni maarufu kwa habari zake katika ukurasa wake wa kwanza.
Huku raia wakisubiri uchaguzi wa siku ya Jumamosi ,gazeti hilo liliweka picha za wagombea wawili wakuu wa uchaguzi huo katika ndoana ya samaki na kumrushia mamba anayeitwa Burt mwenye urefu wa mita 5.1.
Burt alionekana kuifuata picha ya kiongozi wa upinzani Bill Shorten ,lakini baada ya mda akaamua kuitia mdomoni ndoana ya picha ya waziri mkuu Malcolm Turnbull,ikiwa ishara inayoonyesha kwamba ataibuka mshindi katika uchaguzi huo.
''Wanaobashiri tayari wamesema kuwa waziri huyo ataibuka mshindi'', alisema muhariri wa gazeti hilo Matt Williams.
Ubongo wa mamba huyo ni mdogo sana lakini ni miongoni mwa wanyama werevu sana.
Mamba huyo huishi katika mbuga ya wanyama pori ya Crocosaurus Cove na alishiriki katika katika filamu ya Australia Crocodile.
Ni mnyama wa hivi karibuni aliyebainika kuwa mwerevu huku yule maarufu akiwa Pweza Paul,ambaye alifanikiwa kubashiri matokeo ya mechi saba katika kombe la dunia la mwaka 2010 nchini Ujerumani.

Magonjwa ya akili yakithiri Sudan Kusini


Shirika la Kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limesema maelfu ya raia wa Sudan Kusini wanasumbuliwa na kiwewe baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, na walio wengi hawana matarajio ya kupata tiba.Shirika hilo limesema watu walilazimishwa kula nyama ya binaadamu wenzao na wengine walilazimishwa kuipasua miili ya binaadamu wenzao wakati huo wa kivita, vilivyoanza mwishoni mwa mwaka 2013.
Amnesty inasema kwamba katika hali ya kusikitisha Sudan Kusini ina hali mbaya ya ukosefu wa huduma za afya ya akili, ikiwa na madaktari wawili tu magonjwa ya akili wakihudumia idadi ya watu zaidi ya milioni kumi.
Wagonjwa wa magonjwa ya akili mara nyingi wamekuwa wakizuia magerezani.

Messi ahukumiwa ‘kufungwa miezi 21 jela’

Mchezaji nyota wa Argentina na Barcelona Lionel Messi amehukumiwa kifungo cha miezi 21 jela baada ya kupatikana na makosa ya kutumia ulaghai wakati wa ulipaji ushuru, vyombo vya habari nchini Uhispania vinaripoti.
Babake, Jorge Messi, pia amehukumiwa kufungwa jela kwa kuilaghai Uhispania €4.1m (£3.2m; $4.6m) kati ya 2007 na 2009.
Wakati wa kesi, waendesha mashtaka walisema maeneo salama yenye kinga dhidi ya ushuru Belize na Uruguay yaliyumiwa kuficha mapato kutokana na uuzaji wa haki za picha za mchezaji huyo.
Lakini Messi amesema hakufahamu lolote kuhusu masuala yake ya kifedha.
Wawili hao hata hivyo hawatarajiwi kufungwa jela.
Chini ya mfumo wa haki nchini Uhispania, mtu anaweza kutumikia kifungo chochote kilicho chini ya miaka miwili nje ya gereza.
Messi na babake pia wanaweza kukata rufaa katika Mahakama ya Juu nchini humo.

Friday, July 1, 2016

Modem(modulator - den odulator )

A modem ( modulator- dem odulator) is a network
hardware device that modulates one or more carrier
wave signals to encode digital information for
transmission and demodulates signals to decode the
transmitted information. The goal is to produce a
signal that can be transmitted easily and decoded to
reproduce the original digital data. Modems can be
used with any means of transmitting analog signals,
from light emitting diodes to radio . A common type
of modem is one that turns the digital data of a
computer into modulated electrical signal for
transmission over telephone lines and demodulated
by another modem at the receiver side to recover
the digital data.
Modems are generally classified by the amount of
data they can send in a given unit of time, usually
expressed in bits per second (symbol bit/s ,
sometimes abbreviated "bps"), or bytes per second
(symbol B/s ). Modems can also be classified by
their symbol rate, measured in baud . The baud unit
denotes symbols per second, or the number of times
per second the modem sends a new signal. For
example, the ITU V.21 standard used audio
frequency shift keying with two possible frequencies,
corresponding to two distinct symbols (or one bit per
symbol), to carry 300 bits per second using 300
baud. By contrast, the original ITU V.22 standard,
which could transmit and receive four distinct
symbols (two bits per symbol), transmitted 1,200 bits
by sending 600 symbols per second (600 baud)
using phase shift keying .