Recent Posts

PropellerAds

Saturday, July 9, 2016

Sudan Kusini:Idadi ya waliouawa haijulikani


Ripoti kutoka mji mkuu wa Sudan Kusini Juba ,zinasema kuwa mili mingi imepelekwa katika hospitali kuu ya mji huo baada ya ufyatulianaji mkali wa risasi kuibuka karibu na nyumba ya rais siku ya Ijumaa.
Idadi ya watu waliouawa hatahivyo haijulikani.
Ufyatulianaji huo ulianza wakati ambapo rais Salva Kiir na makamu wake Riek Machar walikuwa wakijadiliana kuhusu ghasia siku ya Alhamisi baada ya wanajeshi watano wa serikali kuuawa katika vita vya pande pinzani.

Viongozi wote wawili wametaka kuwepo kwa utulivu.
Ghasia hizo ni mbaya zaidi kuwahi kutokea tangu makamu wa rais Riek Machar kurudi mjini Juba mnamo mwezi Aprili na vilevile zinajri wakati ambapo taifa hilo changa zaidi duniani liko katika harakati za kuadhimisha mwaka wa tano tangu lijipatie uhuru wake.

Related Posts:

  • Rais wa India kuzuru Afrika Rais wa India Pranab Mukherjee, anaanza ziara ya siku sita barani Afrika yenye lengo la kuboresha ushirikiano wa kibiashara. Atatembelea Ghana, Ivory Coast na Namibia. Afrika inatambuliwa kama mzalishaji muhimu wa mafuta na … Read More
  • MAGAZETI YA LEO TZ NA NJE,JUNE 14 Read More
  • Uzito mkubwa hatari kwa utapia mlo Utafiti mpya umeonya juu ya ongezeko la uzito mkubwa wa watu duniani ambao unaweza kusababisa kusambaa kwa kasi kwa utapia mlo. Kwa kawaida,utapiamlo unaweza kuhusishwa na njaa. Lakini katika ripoti hii ya utapiamlo kimata… Read More
  • Magufuli awaapisha Nchemba na Tizeba Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewaapisha mawaziri wapya wa mambo ya ndani na yule wa kilimo siku mbili tu baada ya kutangaza mabadiliko madogo katika baraza lake la mawaziri. Jumamosi iliyopita rais Magufu… Read More
  • 'Waislamu hawafai kuingia Marekani' -Trump Mgombea wa kiti cha urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump, amesema mauaji ya watu 50 katika baa moja ya wapenzi wa jinsia moja huko Orlando inathibitisha msimamo wake kwamba waislamu wapigwe marufuk… Read More