Recent Posts

PropellerAds

Tuesday, July 12, 2016

Moise Katumbi: Serikali ya DRC ilijaribu kuniua

Kiongozi wa upinzani nchini DRC ambaye pia ni
mgombea wa kiti cha urais katika uchaguzi ujao
amesema kuwa serikali ya rais Joseph kabila ilimpa
sumu katika njama ya kumuua.
Mwanasiasa Moise Katumbi wa Jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo anasema kuwa alidungwa
sindano iliyokuwa na sumu nje ya mahakama ya
Lubumbashi mnamo mwezi Mei.
Katumbi anasema haikujulikana sindano hiyo ilikuwa na
nini.
Hata hivyo anasema askari polisi mmoja alimdunga
sindano katika mshikemshike nje ya mahakama polisi
walipofyatua mabomu ya kutoa machozi kwa mashabiki
wake alipokuwa akienda kujibu mashtaka ya kuwaajiri
mamluki kuwa walinzi wake kinyume cha sheria.
Bw Katumbi anasema kuwa madai hayo dhidi yake ni
ya ''upuuzi''.
Hata hivyo kiongozi huyo ambaye ni mkurugenzi mkuu
wa klabu ya TP Mazembe aligonjeka na akalazimika
kukimbilia nje ya nchi ilikupata matibabu.
Katumbi ameiambia shirika la habari la AFP kuwa
alikwenda Afrika Kusini Uingereza na kisha Ujerumani
kutafuta tiba.
Waziri wa mawasiliano bwana Lambert Mende hakujibu
mawasiliano dhidi ya serikali yake lakini kwa siku nyingi
amepuuzilia mbali tuhuma kuwa polisi wa DRC
walimdhuru bwana Katumbi.

Related Posts:

  • What We Can Do in a World Gone Mad What can we do in light of all that is taking place regarding Israel, THE EPICENTER OF THE MIDDLE EAST AND THE WORLD? We can: RECOGNIZE the true nature of the battle in Israel It is, at its root, a spiritual … Read More
  • Why Israel? "A Jew who does not believe in miracles is not a realist." - David ben Gurion, first Prime Minister of the State of Israel The Holocaust and the Rebirth of Israel A Jew who does not believe in miracles is not a real… Read More
  • Wisdom To Endure Life's Vanities - I (8:1-9:18)INTRODUCTION 1. The Preacher (Solomon, 1:1) has been sharing with us counsel for dealing with life... a. Counsel gleaned from his own search for meaning - 7:27 b. Counsel guided by wisdom given him by God - cf. 1:16… Read More
  • Where Did It All Start? The Origins of the Arab-Israeli Conflict It’s not about the land The creation of the State of Israel in 1948 didn’t take a significant amount of land from Middle Eastern Arabs. Israel comprises 0.2 percent of the Middle East’s land mass. (That’s two-… Read More
  • BLESSED ARE THE POOR IN SPIRIT INTRODUCTION: "Blessed are the poor in spirit: for theirs is the kingdom of heaven" (Matthew 5:3). This idea, along with so many others in the Bible, seems so foreign to the modern mind. How can poverty in any form be good… Read More