Recent Posts

PropellerAds

Wednesday, July 6, 2016

Magonjwa ya akili yakithiri Sudan Kusini


Shirika la Kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limesema maelfu ya raia wa Sudan Kusini wanasumbuliwa na kiwewe baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, na walio wengi hawana matarajio ya kupata tiba.Shirika hilo limesema watu walilazimishwa kula nyama ya binaadamu wenzao na wengine walilazimishwa kuipasua miili ya binaadamu wenzao wakati huo wa kivita, vilivyoanza mwishoni mwa mwaka 2013.
Amnesty inasema kwamba katika hali ya kusikitisha Sudan Kusini ina hali mbaya ya ukosefu wa huduma za afya ya akili, ikiwa na madaktari wawili tu magonjwa ya akili wakihudumia idadi ya watu zaidi ya milioni kumi.
Wagonjwa wa magonjwa ya akili mara nyingi wamekuwa wakizuia magerezani.