Recent Posts

PropellerAds

Wednesday, July 6, 2016

Messi ahukumiwa ‘kufungwa miezi 21 jela’

Mchezaji nyota wa Argentina na Barcelona Lionel Messi amehukumiwa kifungo cha miezi 21 jela baada ya kupatikana na makosa ya kutumia ulaghai wakati wa ulipaji ushuru, vyombo vya habari nchini Uhispania vinaripoti.
Babake, Jorge Messi, pia amehukumiwa kufungwa jela kwa kuilaghai Uhispania €4.1m (£3.2m; $4.6m) kati ya 2007 na 2009.
Wakati wa kesi, waendesha mashtaka walisema maeneo salama yenye kinga dhidi ya ushuru Belize na Uruguay yaliyumiwa kuficha mapato kutokana na uuzaji wa haki za picha za mchezaji huyo.
Lakini Messi amesema hakufahamu lolote kuhusu masuala yake ya kifedha.
Wawili hao hata hivyo hawatarajiwi kufungwa jela.
Chini ya mfumo wa haki nchini Uhispania, mtu anaweza kutumikia kifungo chochote kilicho chini ya miaka miwili nje ya gereza.
Messi na babake pia wanaweza kukata rufaa katika Mahakama ya Juu nchini humo.

Related Posts:

  • MAGAZETI YA LEO MAY 3 Read More
  • Mjue Ndovu Ndovu au tembo ni aina za wanyama wenye umbo kubwa kupita wanyamapori wote. Watoto wake wakizaliwa hufikia kg 100 na ndovu mzima huwa na uzito wa tani 2 hadi 5; kimo ni hadi m 4. Kibiolojia ni mamalia. Sehemu ya pekee mwilin… Read More
  • Ranieri kutotazama mechi muhimu ya Spurs Meneja wa Leicester Claudio Ranieri amesema huenda akashindwa kutazama mechi muhimu ya leo jioni kati ya Chelsea na Tottenham. Iwapo Tottenham watashindwa kuondoka na ushindi uwanjani Stamford Bridge, basi Leicester watat… Read More
  • Leicester City mabingwa wapya EPL Klabu ya soka ya Leicester City wameshinda taji la ligi kuu England katika historia inayovutia kwenye ligi hiyo. Suluhu ya 2-2 waliyoipata Tottenham dhidi ya Chelsea siku ya jumatatu usiku ilisababisha mafanikio hayo mak… Read More
  • Mvumbuzi wa PIN alivyoondoka mikono mitupu Je, wajua mtu aliyevumbua nambari ya siri maarufu kama PIN ambayo watu wengi hutumia katika kadi za benki na katika kufanya malipo hakulipwa chochote kutokana na uvumbuzi wake? Mwanamume huyo si mwingine ila ni James Goodf… Read More