Recent Posts

PropellerAds

Tuesday, November 15, 2016

Nigeria yakumbwa na njaa kali

Umoja wa Mataifa umetoa tamko kwamba
wanaijeria wapatao nilioni kumi na nne
wanahitaji misaada ya kibinaadamu
upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo, mahali
ambako maelfu kwa mamia ya watoto wako
kwenye hatari kubwa ya kifo kutokana na
njaa kali na kwamba watoto laki nne
wanahitaji msaada wa dharula.
Inaelezwa kuwa mkoa uliokumbwa na baa
hilo la njaa awali ilikuwa ngome ya zamani
ya kundi la dola ya kiislamu Kiislam, Boko
Haram.Jimbo hilo lilikuwa katika hali tete
kiasi cha kutokufikiwa na misaada ya
kibinaadamu kwa miaka kadhaa sasa
ambapo kwa sasa ndiyo limebainika kuwa na
hali mbaya ya chakula na njaa kali ikiwemo
majimbo ya Borno,Yobe na Adamawa.
Shirika la kuwasaidia watoto la , Unicef,
limesema kwamba inakadiwa kuwa watoto
wapatao elfu sabini na watano wako katika
hatari ya kufa.
Mapema , shirika la misaada ya kitabibu la
madaktari wasio kuwa na mipaka
wamegundua idadi kubwa zaidi ya watoto
walio chini ya umri wa miaka mitano katika
kambi mbili za wakimbizi utafiti ambao
uliainishwa kwa kiasi kikubwa kuwa wa chini
kuliko ilivyotarajiwa, na kwamba
inaaminika robo ya watoto hao walikwisha
kufa .