Recent Posts

PropellerAds

Thursday, August 23, 2018

Malalamiko sita (6) ya Malaika


Image result for angelsKati ya viumbe vyote ambavyo Mungu ameviumba  hakuna kiumbe hata kimoja chenye thamani kumshinda Mwanadamu.
Mwanzo1:1
Hapo mwazo  Mungu aliziumba mbingu  na nchi,
Mwanzo 1:26
Mungu akasema, na tumfanye  mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa Baharini.na ndege wa again,na wanyama na nchi yote pia na kila chenye kutambaa kitaambacho juu ya nchi.
Mawazo ya malaika,
Zaburi 8:4-6.
“Mtu ni kitu gani hata umkumbuke ? Na binadamu hata umwangalie? Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu Umemvika taji ya Utukufu na Heshima,
Waebrania 2:5
“Maana hakuuweka chini ya malaika ulimwengu ule ujao tunaounena ”


Malalamiko  sita (6) ya Malaika
1.kwa nini umkumbuke Mwanadamu
Mwanadamu alipewa nafasi ya kufikiriwa na Mungu kila mahali.
2.Mwanadamu ni nani hata umjali(kwa nini Mungu Umjali Mwanadamu)
3.Umemfanya kuwa karibu na Mungu(kwa nini umemfanya Mwanadamu kuwa rafiki yako)
4.Umempa fahari na Heshimu (Utukufu na Heshima)
5.Umemtawaza juu ya kazi zako zote(Madaraka yote juu ya yote aliyotenda Mungu.)
6.Umetia vitu vyote chini ya mamlaka yake chini ya miguu yake. Waebrania 2:8
Hivyo basi tunaona mtekaji mkuu wa haki ya mwanadamu ni malaika Muasi. Huyu aliasi akiwa mbinguni na ndio mtoa hoja juu ya binadamu.
Sifa za huyu malaika muasi ni:-
Malaika mtiwa mafuta.
Mwili wake ulifunikwa kwa vito.
Kerubi afunikae Ezekiel 28:14.
Aliumbiwa mziki (Lucifer)
Alipotaka kufanya mageuzi ya kutaka kuchukua nafasi ya Mungu, Mungu alimshusha Duniani na majina yake yalifuatanana na kazi zake .
Majina hayo ni:-
1.shetani.
Mshindani wa Mungu.
 ufunuo 12:7
Kulikuwa na vita mbinguni;Mikaeli na Malaika zake wakapigana na Yule joka, Yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; nao hawakushinda wala akatupwa yule mkubwa ,nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na shetani, audanganyae ulimwengu wote;akatupwa hata chini na malaika zake wakatupwa  pamoja nae.
2,Ibilisi
Mshitaki wa uongo, mdanganyifu.
1 Mambo ya nyakati 21:3
Mbona awe sababu ya hatia ya Israel?
Mathayo 4:10
“ndipo yesu alipomwambia Nenda zako shetani kwa maana imeandikwa,msujudie Bwana Mungu wako umwabudu yeye peke yake”
3.Beelzebuli.
Mungu wa mafanikio ya haraka haraka.Mungu wa mbolea. Shetani ni  adui halali na mpinzani  wa haki zote ambazo Mungu aliwandalia wanadamu.
Shetani huwa hadaa wanadamu kwa udanganyifu wa mali na maisha mazuri ya kitambo lakini mwisho wake ni mauti na majuto makuu.
Mathayo 12:24

4.joka
Kulikuwa na vita mbinguni;Mikaeli na Malaika zake wakapigana na Yule joka, Yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; nao hawakushinda wala akatupwa yule mkubwa ,nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na shetani, audanganyae ulimwengu wote;akatupwa hata chini na malaika zake wakatupwa  pamoja nae.
ufunuo 12:7