Recent Posts

PropellerAds

Saturday, April 15, 2017

Korea kaskazini: tupo tayari kwa vita kamili.

Korea Kaskazini imeionya Marekani kutoanzisha vitendo vya uchokozi katika eneo la Korea ikisema kuwa iko tayari kulipiza kisasi kupitia mshambulio ya kinyuklia.
Taifa hilo limesema hivyo wakati ambapo kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un, amehudhuria gwaride la heshima katika mji mkuu wa Pyong yang, akiadhimisha siku ya kuzaliwa ya babu yake, marehemu Kim II-Sung, ambaye ni mwanzilishi wa taifa hilo.
"tumejiandaa kwa vita kamili'' ,alisema Choe Ryong-hae, anayeaminika kuwa mu wa pili mwenye uwezo mkubwa katika taifa hilo.
''Tuko tayari kulipiza kisasi na mashambulio ya Nuklia kwa mbinu zetu dhidi ya shambulio lolote la Kinyuklia''.
Huku kukiwa na wasiwasi kwamba Korea Kaskazini inakaribia kupata ufanisi wa kukamilisha silaha za Kinyuklia, Gwaride la Jumamosi ilikuwa fursa kwa bwana Kim kuonyesha uwezo wa kijeshi wa taifa hilo.
Vifaa vilivyoonyeshwa kwa mara ya kwanza vilikuwa vile vilivyotajwa kuwa manuwari za Pukkuksong ,makombora ya masafa marefu yanayoweza kwenda kwa takriban kilomita 1000.
Wachanganuzi wa vifaa vya kijeshi pia wanasema kuwa kuna makombora mawili mapya yanayoweza kurushwa kutoka bara moja hadi jingine, lakini haijulikani iwapo yamefanyiwa majaribio.
Kulikuwepo na sherehe za kawaida, kama vile mamia ya wanajeshi kupiga gwaride na msafara wa magari ya kivita huku yakiwa yamebeba silaha kama vile makombora.
Maonyesha ya silaha nyingi yanaendelea nchini humo wakati ambapo kuna hali ya uhasama kati ya Korea Kaskazini na Marekani kufuatia mazoezi ya makombora ya kinyukilia yanayoandaliwa na Korea Kaskazini.
Hali ya wasiwasi imekumba eneo la Korea kwa ujumla kufuatia majaribio kadhaa ya makombora ya kisasa na Korea Kaskazini na mapema Jumamosi shirika la habari la taifa hilo lilionya Marekani kusitisha kiherehere chake cha vitisho vya kijeshi.
Marekani imetuma meli kadhaa za kivita katika Rasi ya Korea.
Hiyo jana waziri wa mashauri ya kigeni wa Uchina alionya kuwa vita vyovyote kati ya Korea Kaskazini na Marekani havitamfaidi ye yote.

Related Posts:

  • The Greatest Thing You Can Do with Your Life One of the most wonderful and hopeful things you can know about yourself and your life is captured in a rather unassuming, simple sentence: Only let each person lead the life that the Lord has assigned to him, and to whi… Read More
  • Importance of the Heart It was almost forty years ago, but I remember it like it was yesterday. At the end of an evening church meeting, we flowed seamlessly into an “afterglow service.” For the first time in my life I heard and sang these words… Read More
  • What Is the Gospel? What Is the Gospel? What is the gospel? I’ll put it in a sentence. The gospel is the news that Jesus Christ, the Righteous One, died for our sins and rose again, eternally triumphant over all his enemies, so that there… Read More
  • Hearts That Hear No matter which way my mind turns these days, I cannot escape the absolutely unique and essential role that the Bible plays in God’s purpose for the universe, and for history, and for the church, and for Christian schools,… Read More
  • Even Evil Points Us to God A great evil happens in the world and you’re involved. Say something like a holocaust with six million murders. Or say a Soviet Stalinist cleansing in the gulag with ten times the murders of the Holocaust. Say you’re invol… Read More