Recent Posts

PropellerAds

Sunday, May 28, 2017

KICHECHE au CHECHE (African polecat) ni mnyama mdogo mwenye vituko vingiÂ

KICHECHE au CHECHE (African polecat) ni mnyama mdogo mwenye vituko vingi ambavyo huwashangaza watu wengi na moja ya kituko hicho ana uwezo wa kujamiana mara nyingi zaidi  kwa siku na wana milio maaluma kila wakitaka kujamiana.
Kicheche ni mnyama anayepatikana katika  sehemu ya jangwa la sahara Barani   Afrika,ukanda wa savana na mnyama huyu ni adimu sana  kupatikana katika  misitu mikubwa kama ya  Congo na  maeneo ya pwani.
Mnyama huyu anafanana sana na NGUCHIRO  ana urefu wa sentimeta 60 urefu huo   una jumlisha mwili na mkia wake, na  mkia pekee una urefu wa sentimeta 20.chakula kikubwa cha kicheche ni ndege,nyoka,mijusi,chura,wadudu  na wanyama wengine wadogo kama panya nk.
Wakati wa kukabilina na maadui,mnyama huyo hutoa harufu kali kwa kujamba na kuwafanya maadui kugaili kumkamata  na wazungu humuita “Father of  stinks kutokana na harufu kali anayo toa wakati akijihami na maadui.
Pia kicheche ana tabia ya kuinua mkia wake kwa kubinua mgongo ili aonekane mkubwa baada ya kumuona adui yake  kwa lengo la kumtisha na mara nyingi hupenda kula kila wakati na ana uwezo wa kuishi miaka 13.
Ni namna gani hufanikisha mawindo yake?kumekuwa na dhana nyingi sana wengine wakizani hutumia sehemu ya haja kubwa kukamata ndege au kuku,lakini utafiti unaonyesha kuwa  hutumia miguu yake ya nyuma iliyoimara (badala ya miguu ya mbele) kumkatama mnyama  mdogo au ndege na kisha kumbana kwa ufundi mkubwa.