Recent Posts

PropellerAds

Wednesday, May 17, 2017

Vyakula 4 bora kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa.

Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa.

Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum.

Spinachi
 Image result for spinach picture
Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka.

Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele.

Chai ya Kijani (Green tea)
 Image result for green tea picture
Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.

 Mafuta ya samaki
 Image result for fish oil picture
 Zipo aina nyingi za mafuta ya samaki. Lakini mafuta ya samaki wenye asidi ya Omega-3 yana virutubisho ambavyo huongeza kiwango cha ‘dopamine’ kwenye ubongo.

 Dopamine ni eneo la ubongo linalofanya kazi ya kudhibiti faraja na hisia.  Kama dopamine itaongezeka basi mwanamke hujisikia kuridhika anapokuwa na mwenza wake.

Chokoleti
 
 Pamoja na utamu wake, lakini ‘chocolate’ ina virutubisho na madini ya magnesium ambayo humfanya mwanamke kuridhika. Pia huufanya ubongo wa mwanamke kutulia kwa kuondoa msongo wa mawazo. Msongo wa mawazo ukiisha ni rahisi kwa mwanamke kupata hamu ya tendo la ndoa.

Related Posts:

  • Amuua mfanyakazi akidhani ni ngiri Afrika Kusini Watu nchini Afrika Kusini wamegadhabishwa, kufuatia taarifa za mwanamme mmoja, ambaye analaumiwa kwa kumuua kwa kumpiga risasi mfanyakazi wa shamba, akidhani kuwa mtu huyo ni ngiri. Stephen Hepburn alifikishwa mahakamani… Read More
  • Watu zaidi wakamatwa kufuatia kifo cha Kim Jong-namWashukiwa wawili zaidi wamekamatwa kuhusiana na kifo cha Kim Jong-nam, ambaye ni ndugu wa kambo wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un nchini Malaysia. Mshukiwa mmoja mwanamke raia wa Indonesia na mwanamume raia wa Malays… Read More
  • Kijana aponzwa na Adolf Hitler nchini Austria Polisi nchini Australia wametangaza kwamba imemkamata kijana mwenye umri wa miaka 25, ambaye alivalia mavazi yanayofanana na aliyewahi kuwa matawala wa manazi Adolf Hitler kwa makosa ya kuutukuza utawala na enzi ya wanaz… Read More
  • Viongozi wa madaktari Kenya wafungwa jela mwezi mmoja Mahakama ya masuala ya wafanyakazi nchini Kenya imewahukumu viongozi saba wa chama cha wahudumu wa afya (KMPDU) kufungwa jela mwezi mmoja kwa kukaidi agizo la kumaliza mgomo ambao umedumu kwa zaidi ya miezi miwili. Jaji … Read More
  • Baraza la makardinali lamshangaa Papa Baraza kuu la ushauri linaloongozwa na kiongozi mkuu wa kanisa katoliki ulimwenguni Papa Francis , limechukua hatua isiyokuwa ya kawaida ya kutoa taarifa yenye kuonesha kuwa linamuunga mkono. Hali hiyo inafuatia upinzan… Read More