Recent Posts

PropellerAds

Sunday, May 28, 2017

MAAJABU YA SAMAKI WENYE NGUVU YA UMEME(ELECTRIC FISH)






SAMAKI anayefahamika kwa jina la kimombo la Electric eel ni moja ya samaki wenye nguvu za umeme wanaopatikana katika  maeneo mbalimbali hapa duniani.
Samaki huyo anapatikana  katika mto Amazoni katika bara la Amerika kusini anatajwa kuwaana uwezo wa kuzalisha  nguvu kubwa ya  umeme mwilini mwake  kwenye ogani maalum za mwili wake.
Nguvu hizo za umeme za samaki huyo aina ya Electric eel zinatajwa kuwa kwenye misuli na seli za mwili wake na mara nyingi nguvu hiyo ya umeme huitumia kwajili ya kujihami na maadui na hutumia wakati akitafuta chakula ambapo hutumia nguvu hiyo ya umeme kwajili ya kuwaua viumbe wakiwemo samaki wa kawaida kwajili ya kitoweo.
Maajabu ni kuwa  samaki aina ya Electric eel anayepatikana  katika mto amazoni kusini mwa bara la Amerika mwenye nguvu ya umeme inayofikia volt 500 na samaki aina ya  Electric catfish anayepatikana katika mto Nile nchini Misri katika bara la Afrika mwenye nguvu ya  umeme inayofikia volt 350 ndiyo samaki wanaotajwa kuwa  na uwezo wa kumuua hata  binadamu   au mnyama kama Pundamilia.
Takwimu za watalaam mbalimbali duniani zinaonyesha kuwa kuna samaki zaidi ya mia mbili (200) wenye nguvu ya umeme na aina hii ya samaki wenye nguvu ya umeme wanapatikana  katika bahari na mito.
Katika bara la Afrika Samaki hawa wanapatikana zaidi katika maeneo ya tabia ya kitropiki na baadhi ya maeneo ambayo unaweza kuwaona samaki hao ni katika Ziwa Tanganyika,Mto Nile  nchi ya Misiri na katika mto Ogooue nchini Gabon na baadhi ya mito katika nchi za Afrika ya kati.
Pia samaki hao wenye nguvu ya umeme wanapatikana kwa wingi zaidi katika bara la Amerika kusini katika mito ya Amazon na Orinoco na ni samaki wanaotajwa kuwa wamekuwa wakiuwa viumbe wengi sana majini.
Na katika bahari samaki hao wanapatikana katika bahari ikiwemo ya  Pasific na katika bahari za  Mediterranean na  Caribbean  ingawa samani wengi wa baharini hawana nguvu kubwa ya umeme kama samaki wa kwenye mito.
Jambo la kukumbuka ni kuwa samaki hawa wenye nguvu ya umeme kwamjibu wa taarifa za kitalaam ni kuwa hawafai kwajili ya kitoweo.
Samaki hao wenye nguvu ya umeme wanatajwa kuwa ni miongoni mwa  samaki (10) hatari sana duniani,wakiwemo  Lion Fish,. Piranha. Bull Shark. 4 Great White Shark, Stone Fish. Puffer Fish, Box Jelly Fish na  Electric Eel.