Recent Posts

PropellerAds

Tuesday, June 13, 2017

Wekeza katika maarifa

"Until your brain sweat, you won't experience swiftness" Image result for family reading picture
Katika kitabu cha Hosea 4:6 imeandikwa “watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa…” Inawezekana umesikia mara nyingi sehemu hii; swali ambalo nataka tujiulize kwa pamoja na kulitafakari ni, je kwanini Mungu hamzuii au hajamzuia muangamizaji wa watu wake? Kumbuka hawa wanauhusishwa hapa si wapagani bali ni watu wa Mungu; hivyo swali linabaki kwanini Mungu hajamzuia mwangamizaji na ameacha mpaka wanaangamizwa?
Isaya anandika, “Kwa sababu hiyo watu wangu wamechukuliwa mateka, kwa kukosa kuwa na maarifa;...” Isa5:13. Hapa pia nataka tujiulize kwa pamoja, kwanini Mungu hakumzui mtekaji au watekaji  mpaka watu wake wanatekwa? Kwanini watu wake wanatekwa mbele yake na ameacha mpaka wamechukuliwa mateka?
Dr. David Oyedepo amewahi kusema, “God cannot help you and I beyond our level of knowledge of Him” yaani Mungu hataweza kutusaidia zaidi ya kiwango chetu cha maarifa (ufahamu) tulichonacho (Tafasiri isiyo rasmi). Mpaka umeujua na kuelewa ‘ukweli’ huu hauwezi kuelewa pale Mfalme Suleimani aliposema na kusisitiza juu ya kuwekeza katika maarifa na ufahamu, “Bora hekima, basi jipatie hekima; naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu (wisdom is supreme, therefore get wisdom; though it may cost all you have get understanding)”.Mith 4:7
Petro anasema, uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu VYOTE, lakini tunauwezo wa kuvifikia (experience in our lives) vitu hivyo kwa njia ya maarifa katika yeye (2Petro1:3, msisitizo umeongezwa). Kumbuka, Mpaka pale umejitoa kuwekeza katika maarifa na ufahamu katika eneo husika, hautaweza kubadili nafasi uliopo, iwe katika eneo la elimu, uchumi, biashara, uongozi, uhusiano, kazini.. N.k (Until you give yourself to the investment in knowledge and understanding, you won’t change your position)
Uwekezaji katika maarifa unahitaji uwekezaji wa muda, juhudi na rasilimali zingine ili kupata matokeo bora katika maisha yetu ya kila siku. Mpaka umewekeza katika maarifa, maisha yako yanabaki kuwa mawindo mepesi kwa muangamizaji na mtekaji. Ni ‘kweli’ ulioijua pekee katika eneo husika (specific) ndio itakayokufanya au kuwezesha kuishi huru katika eneo hilo. Yh 8:32! Kumbuka, maombi hayawezi kubadili sehemu ya maarifa; kama eneo hilo linahitaji maarifa ili uweze kuvuka, hata kama utafunga na kuomba bila maarifa hayo hauwezi kubadili mahali ulipo (Prayer cannot replace the role of understanding and knowledge)!
Mwenyehekima mmoja anasema, asilima kubwa ya changamoto alizonazo mtu majibu yake yapo kwenye vitabu na semina mbali mbali ambazo alikuwa na nafasi ya kuyafikia maarifa lakini hakufanya hivyo kwa sababu yoyote ile.