Recent Posts

PropellerAds

Thursday, March 16, 2017

Kwa Picha: Ndege ya wanawake pekee kutoka Malawi yatua Tanzania

Wahudumu wa ndege ya Malawi
Shirika la ndege la Malawi, Malawi Airlines, limefanikiwa kukamilisha safari ya ndege iliyosimamiwa na wanawake pekee.
Ndege hiyo imetua katika uwanja wa Mwalimu Julius Nyerere mjini Dar es Salaam.
Marubani na wasaidizi wa abiria kwenye ndege hiyo wote walikuwa wanawake, na ni mara ya kwanza kwa shirika hilo kuandaa safari kama hiyo.
Ndege hiyo ilianza safari yake mjini Blantyre na itatua kwa muda Lilongwe kabla ya kuelekea Dar es Salaam.
Shirika hilo la ndege, lilisema lengo la kuandaa safari hiyo ni kufanikisha ulimwengu ambao "unakumbatia jinsia zote"MarubaniWahudumu wa ndege ya MalawiNdege hiyo ilikuwa chini ya Kapteni Yolanda Kaunda akisaidiwa na Lusekelo Mwenifumbo.
Bi Mwenifumbo, 24, ambaye alisomea urubani jijini Addis Ababa, Ethiopia ameambia Munira Hussein wa BBC kwamba alihamasishwa kuwa rubani na babake ambaye pia alikuwa rubaniWahudumu wa ndege ya MalawiWahudumu wa ndege ya MalawiWahudumu wa ndege ya MalawiNdege hiyo uwanja wa ndege wa wa kimataifa wa Mwalimu Julius NyerereNdege ya Malawi