Recent Posts

PropellerAds

Monday, February 13, 2017

Viongozi wa madaktari Kenya wafungwa jela mwezi mmoja

Maandamano ya wanafunzi
Mahakama ya masuala ya wafanyakazi nchini Kenya imewahukumu viongozi saba wa chama cha wahudumu wa afya (KMPDU) kufungwa jela mwezi mmoja kwa kukaidi agizo la kumaliza mgomo ambao umedumu kwa zaidi ya miezi miwili.
Jaji Hellen Wasilwa amesema viongozi hao hawajatoa sababu ya kutosha kuonesha ni kwa nini hawajamaliza mgomo huo
Ameamuru mazungumzo ya kumaliza mgomo huo yaendelee.
Jaji Wasilwa alikuwa awali amewapa viongozi hao muda wa wiki mbili kumaliza mgomo huo, na baadaye akawaongezea siku tano.
Mazungumzo ya kumaliza mgomo huo hata hivyo hayakuzaa matunda kipindi hicho.
Madaktari wamekuwa wakiitaka serikali kuheshimu makubaliano ya mwaka 2013 ya kuwaongezea mishahara.
Wamekataa mshahara walioongezewa na serikali wa asilimia 40 wakisema kuwa ni wa chini kuliko ule walioafikiana mwaka 2013.
Karibu madaktari na wauguzi 5000 kutoka hospitali 2000 za umma, walianza mgomo wiki ya kwanza ya mwezi Desemba na wagonjwa wamekuwa wakikosa matibabu.

Related Posts:

  • France and Germany back Libya unity cabinet   The French and German foreign ministers have made an unannounced visit to Libya, in a show of support for the country's new UN-backed government. In Tripoli, Germany's Frank-Walter Steinmeier said the EU was ready… Read More
  • MAGAZETI YA LEO APRIL 18   … Read More
  • Korea Kaskazini kulipua bomu la nyuklia Korea Kusini imesema imepata dalili kwamba Korea Kaskazini inajiandaa kufanya jaribio la tano la bomu la nyuklia, Rais Park Geun-hye amesema. Hakufafanua zaidi kuhusu dalili hizo, lakini ameagiza jeshi la nchi yake kuwa t… Read More
  • Kunguni sasa ni sugu kwa dawa Huenda kunguni wakawa sugu kwa dawa, hali ambayo itasababisha wadudu hao kuwa na uwezo kuhimili makali ya dawa ya kuua wadudu. Idadi ya watu inayozidi kuongezeka na safari za kimataifa zimesadia mdudu huyo kuwa kero kwenye … Read More
  • Annan: Nkurunziza hakustahili kuwania urais Aliyekuwa Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa bwana Kofi Annan amemkosoa rais wa Burundi Pierre Nkurunziza kwa kuwania muhula wa tatu. Bw Annan amesema Nkurunziza anafahamu vyema kuwa ni kinyume cha katiba ya taifa hilo kuwa… Read More