Recent Posts

PropellerAds

Sunday, February 19, 2017

Jeshi la Marekani laanzisha doria Kusini mwa Bahari ya China

Meli ya Marekani ya kubeba ndege za kivita ya USS Carl Vinson
Meli ya Marekani ya kubeba ndege za kivita ya USS Carl Vinsion imeanza kile kinatajwa kuwa oparesheni za kawaida kusini mwa bahari ya China, ikiandamana na meli zingine za kivita.
Oparesheni hiyo inakuja siku chache baada ya wizara ya mashauri ya nchi za kigeni ya China kuionya Marekani kwa kupinga uhuru wa China katika eneo hilo.

China inadai kumiliki maeneo kadha ya eneo la bahari ya kusini mwa China.
Imekuwa ikijenga visiwa bandia vilivyo na viwanga vya ndege kwa miaka kadha.
China imejenga visiwa bandia kusini mwa bahari ya China
Meli hiyo ya kubeba ndege za kijeshi ilipitia mara ya mwisho eneo la kusini mwa bahari ya China miaka miwili iliyopta, wakati wa mazoezi na jeshi la Malaysia, na imefanya safari 16 kwa miaka 35 ya huduma yake.
Muda mfupi baada ya Donald Trump kuchukua uongozi mwezi Januari, utawala wake uliapa kuizuia China kudhibiti eneo la Kusini mwa bahari ya China.
Siku ya Jumatano msemaji wa wizara ya mashauri ya nchi za kigeni nchini China Geng Shuang, aliitaka Marekani kutochukua hatua ambayo itapingauhuru na usalama wa China.
 Kusini mwa habari ya China