Recent Posts

PropellerAds

Wednesday, February 15, 2017

Amuua mfanyakazi akidhani ni ngiri Afrika Kusini

Ngiri
Watu nchini Afrika Kusini wamegadhabishwa, kufuatia taarifa za mwanamme mmoja, ambaye analaumiwa kwa kumuua kwa kumpiga risasi mfanyakazi wa shamba, akidhani kuwa mtu huyo ni ngiri.
Stephen Hepburn alifikishwa mahakamani ili kujibu mashtaka ya mauaji.
Yeye na mwenzake wa kike walikuwa wakiwawinda ngiri kwenye shamba moja lililo mkoa wa Limpopo kaskazini siku ya Jumamosi, wakati Jan Railo ambaye alikuwa na umri wa miaka 23 aliuawa
Msemaji wa Polisi Motlafela Mojapelo aliiambia BBC kuwa Bwana Hepbaun, alikamatwa siku ya Jumatutu.
Mojapelo aliongeza kusema kuwa bwana Hepburn alisema kuwa aliafyatua risasi eneo ambapo alisikia sauti alipokuwa akiwinda, na alipoenda kuangalia akapata kuwa ni mtu alikuwa amelala chini.
Wanachama wa tawi la chama cha ANC eneo hilo ambao waliofika mahakamani walisema hawaamini ikiwa mauaji hayo yalikuwa ya kimakosa.

Related Posts:

  • Mvumbuzi wa PIN alivyoondoka mikono mitupu Je, wajua mtu aliyevumbua nambari ya siri maarufu kama PIN ambayo watu wengi hutumia katika kadi za benki na katika kufanya malipo hakulipwa chochote kutokana na uvumbuzi wake? Mwanamume huyo si mwingine ila ni James Goodf… Read More
  • Waliofariki mkasa wa jengo Nairobi wafika 21 Idadi ya watu waliofariki baada ya jengo la ghorofa sita kuporomoka Nairobi imefika 21 baada ya miili mingine mitano kufukuliwa kutoka kwenye vifusi. Waokoaji wamewanusuru watu 135 huku wengine zaidi ya 90 wakiwa bado haw… Read More
  • Miili ya waliotoweka miaka 16 iliyopita yapatikana Miili ya wakwea milima wawili kutoka Marekani waliotoweka katika milima ya Himalaya miaka 16 iliyopita imepatikana. Mkwea milima maarufu duniani Alex Lowe alikuwa akikwea katika kilele cha Shishapangma chenye urefu wa 8,0… Read More
  • Vardy mchezaji bora wa mwaka Uingereza Mshambuliaji wa Leicester Jamie Vardy ametawazwa mchezaji soka bora wa mwaka na chama cha waandishi wa kandanda Uingereza. Mshambuliaji huyo wa Uingereza alipata 36% ya kura zilizopigwa na wanahabari 290 na kuwashinda we… Read More
  • Vardy mchezaji bora wa mwaka Uingereza Mshambuliaji wa Leicester Jamie Vardy ametawazwa mchezaji soka bora wa mwaka na chama cha waandishi wa kandanda Uingereza. Mshambuliaji huyo wa Uingereza alipata 36% ya kura zilizopigwa na wanahabari 290 na kuwashinda we… Read More