Recent Posts

PropellerAds

Tuesday, February 28, 2017

unyanyasaji wa watoto wahamiaji libya wakithiri

UNICEF inasema kuwa watoto hunyanyaswa Libya katika harakati za kuelekea Itali
Umoja wa Mataifa umeonya kwamba idadi kubwa ya watoto wanaendelea kuhatarisha maisha yao, kwa kuvuka bahari ya mediterania kutoka Libya hadi Italia.
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia watoto UNICEF, linasema watoto 26,000, wengi wao wakiwa bila walezi, walivuka bahari ya mediterania mwaka jana.
Idadi hiyo ni mara dufu ikilinganishwa na mwaka 2015.
 Watoto hukabiliwa na tisho la kufnywa makahaba na magenge ya uhalifu
Katika ripoti mpya, UNICEF, inasema watoto hao wanadhulumiwa na kunyanyaswa kimapenzi na walanguzi wa binadamu, japo huwa hawatoi ripoti kwa polisi kwa hofu ya kutiwa mbaroni na kurejeshwa Libya.