Recent Posts

PropellerAds

Sunday, February 19, 2017

Waziri mkuu akuta ya ajabu Minjingu

Babati.Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema haridhiki na hali aliyoikuta kwenye kiwanda cha kutengeneza mbolea cha Minjingu baada ya kubaini kuwa wanatumia mifuko yenye lebo ya Kenya wakati mbolea hiyo inazalishwa hapa nchini.
Kutokana na hilo, Waziri Mkuu amewataka wamiliki wa kiwanda hicho waandike barua kwa Rais John Magufuli kabla hajamaliza ziara yake Jumatano, Februari 22, 2017 apate nakala ya barua hiyo.
Ametoa agizo hilo leo baada ya kutembelea kiwanda hicho kilichopo wilayani Babati akiwa katika siku ya tatu ya ziara yake mkoani Manyara. Waziri Mkuu amerejea Babati leo akitokea Dar es Salaam ambako alikuwa na ratiba za kitaifa.
“Nilikuja kukagua kiwanda baada ya kupokea malalamiko kuwa mbolea hii haikubaliki huko vijijini. Watafiti wameonyesha kuwa ikitumika inasaidia kutoa mazao mengi. Lakini wakati niko kiwandani nimekerwa kukuta mifuko ya kupakia mbolea hii ina anuani ya Nairobi, Kenya wakati mali ghafi inatoka Tanzania,” amesema.
“Ni kwa nini mifuko hii ina anuani ya Kenya? Hapa tulipaswa tuone anuani ya Babati! Je mlipata kibali kutoka serikalini? Tena kuna lebo ya TBS. Kwa nini Tanzania haionekani? Kwani malighafi iko Kenya? Haiwezekani, ni lazima uandike barua na uombe radhi kwa Mheshimiwa Rais Magufuli. Yeye anahimiza ujenzi wa viwanda ndani ya nchi, halafu ninyi mnafanya hivyo?”
Akiwa ndani ya kiwanda hicho, Waziri Mkuu alikuta baadhi ya mifuko ya mbolea ikiwa imeandikwa: ‘County Government of Bungoma’, ina nembo ya Serikali ya Kenya, na anuani ikionyesha kuwa mbolea hiyo imetengenezwa na kiwanda cha mbolea cha Minjingu lakini anuani inasomeka P. O Box 2941 – 00200 Nairobi, Kenbro Industrial Park, Mombasa Road; namba ya simu +254-20-6000-970 lakini mifuko hiyo pia ina muhuri wa TBS.

Related Posts:

  • What Grieving People Wish You Knew at Christmas “Happy Thanksgiving!” “Merry Christmas!” “Happy New Year!” As the end of the year approaches, everywhere we turn someone is telling us we should be happy. But for those who’ve recently lost someone they love, the holid… Read More
  • If I Only Knew Why I contracted polio long after it was supposedly eradicated. The doctor misdiagnosed my symptoms because she had never seen polio before. And the wrong diagnosis led to widespread paralysis. With a childhood spent largely … Read More
  • God Will Fulfill His Purpose for You “I cry out to God Most High, to God who fulfills his purpose for me” (Psalm 57:2). David states two basic facts in this verse: God has a purpose for him and God will fulfill that purpose. Both these truths combine to… Read More
  • Do I Love God for His Gifts or for Who He Is? Well first, I think it is absolutely crucial in pursuing that interaction with God to get really clear in our mind and in our heart that there is a huge and important difference between enjoying a person who gives gifts a… Read More
  • Into the Darkness He Came Into the world, on a nondescript night, in a small town grown weary with oppression and centuries of unfulfilled prophetic expectation, in an obscure shelter no one would have thought to look for him, in the care of poor… Read More