Baraza kuu la ushauri linaloongozwa
na kiongozi mkuu wa kanisa katoliki ulimwenguni Papa Francis ,
limechukua hatua isiyokuwa ya kawaida ya kutoa taarifa yenye kuonesha
kuwa linamuunga mkono.Katika taarifa yake, mshauri mwandamizi wa baraza la ushauri la Makardinali walirejelea tukio la hivi karibuni ingawa hawakufafanua zaidi, wakitilia maanani suala hilo kuwa linamuunga mkono papa na mafundisho yake.





