Recent Posts

PropellerAds

Tuesday, February 28, 2017

Mambo yatakayo kufanya ukose heshima kwenye jamii yako

Image result for disrespect picture 
Hakuna kitu kibaya maishani kama kuonekana upo katika daraja la chini na mtu wa kudharaulika kwenye jamii unayoishi. Kisaikolojia kuna madhara makubwa.

Ni imani yangu kuwa kila mwanadamu timamu anapenda kuheshimiwa lakini wengi wetu tunashindwa kupata heshima tunayoitaka kwa sababu hatufahamu jinsi ya kuishi mbele ya wenzetu.

Kitaalamu, hakuna jambo ambalo hutokea maishani bila sababu maalumu hivyo hata kudharauliwa kwako au kwetu ndani ya jamii tunayoishi kunatokana na jinsi tunavyoenenda.

Njia za kukusaidia kurejesha heshima yako kwa kuperuzi na wewe baadhi ya dokezo muhimu zinazoweza kukusaidia kujitambua na kuweza kuyaepuka maisha ya kudharauliwa.

1. Muonekano.
Kwanza kabisa ni jinsi unavyoonekana. Muonekano ninaouzungumzia hapa ni usafi wa mavazi na mwili kwa ujumla. Hata siku moja hakuna mchafu anayeheshimika katika jamii anayoishi hata kama ana kipaji kikubwa kiasi gani.

Kwa hiyo uchafu wa mavazi na mwili huchangia mtu kudharauliwa katika jamii anayoishi.

Linaweza kuwa jambo dogo sana lakini ni moja kati ya sababu kubwa inayochangia kuporomoka kwa thamani yako mbele ya wenzako.

2. Mazungumzo.
Hapa naomba nieleweke kuwa unachokizungumza kinaweza kukujengea heshima au kukubomolea heshima. Kauli zisizo na busara zitakufanya udharaulike kwa kila mtu. Uropokaji usiokuwa na mantiki huchangia kuporomosha heshima yako hasa kama utakuwa muongeaji zaidi. Biblia inasema penye wingi wa maneno hapakosi uovu.

3. Utendaji wako wa Kazi.
Ndugu zangu, siku zote heshima ya mtu ni kazi. Watu wengi hawapendi kufanya kazi kwa bidii huku wengine wakijiendekeza kwa tabia ya kuombaomba, jambo hilo halifai kwa vile huchangia kubomoa heshima yako mbele ya jamii. Fanya kazi usiishi bila kujishughulisha.

4. Kutotimiza ahadi.
Kama una tabia za kuahidi mambo halafu unashindwa kuyatekeleza, basi unajiweka katika nafasi mbaya ya kutunza heshima yako katika jamii unayoishi. Bora ukwepe kutoa ahadi kuliko kuahidi na kutotimiza.

5. Sifa zisizo na maana.
Nakumbuka msemo mmoja kutoka kwa mwandishi mwandamizi aliyekuwa mtaalamu wa falsafa za maisha, marehemu Adolf Balingilaki, ambao unasema kwamba: “Ukitafuta heshima kwa gharama ya juu, basi utalipwa dharau kwa bei nafuu.”

Msemo huu unamaanisha nini? Siku zote ukiwa unafanya mambo yako kwa ajili ya kusifiwa au mazungumzo yako kuwa ya kujiinua, watu watakudharau.

6. Kutokuwa mwaminifu.
Suala la uaminifu ni pana, kuna uaminifu wa fedha, siri, dhamana na mambo kama hayo, hivyo ni vema kila unachoaminiwa lazima ukitunze kwani ukiwa mtu wa kuvunja uaminifu fahamu kuwa utashusha heshima yako

Related Posts:

  • Springs of Life Will Flow And from this new heart of gladness, surpassing all the joys of the world, flow all springs of life (Proverbs 4:23). Out of the abundance of this heart of new gladness, the mind thinks new thoughts, the will resolves new d… Read More
  • You Have a Responsibility to Receive Suppose I’m hungry for a greater portion of peace, a greater portion of tenderness, a greater portion of kindness, a greater portion of sweet enjoyment of Jesus with total authenticity and not watching myself enjoy but just … Read More
  • God’s Light Overcomes Our Blindness If those are the objective blessings of being in the light of God’s face, what are the subjective effects when this light brings us to God, opens our eyes, pours his delight over us, and makes us a blessing to the nation… Read More
  • ‘Let Your Face Shine’ So what does it mean for us when the light of God’s face is lifted up upon us? Let’s widen our lens and see how this phrase is used in the Psalms. Psalm 80:3 — “Cause us to return, O God; let your face shine, t… Read More
  • Seven Ways to Quench the Spirit If the apostle Paul himself had not warned us about quenching the Spirit, who among us would have thought it was possible (1 Thessalonians 5:19–22)? To suggest that the omnipotent Spirit of God could ever be quenched, and … Read More