Recent Posts

PropellerAds

Thursday, January 26, 2017

Mwanamume afa maji huku watu wakimcheka Italia

Mwanamume mmoja raia wa Gambia alikufa
maji huku watu wakitazaka katika eneo la
Venice's Grand Canal nchini Italia.
Gazeti la Times la nchi hiyo linasema kuwa
watu katika mji huo walipiga picha kisa
hicho huku wakicheka na kumtupia maneno
ya ubaguzi wa rangi Pateh Sabally mwenye
umri wa miaka 22.
"Endelea, rudi nyumbani," mmoja wao
aliongea kwa sauti.
Kulingana na shirika la Reuters, majaji nchini
Italia wameanzisha uchunguzi baada ya
video iliyonaswa kwa kutumia simu ya mkoni
siku ya Jumapili kuchapishwa kwenye
mitandao.
Hakuna mtu aliyejaribu kuruka kwenye maji
hayo yenye baridi kumsaidia bwana Sebally,
ambaye anaripotiwa kuwasili nchini Italia
miaka miwli iliyopita.
Lakini vifaa vya kuokoa maisha viliruswa
kwenye maji karibu na mahala alikuwa laniki
hakuonekana kuvifikia, na kuzua uvumi kuwa
alikuwa anataka kujiua.
"Yeye ni mjinga, anataka afe," mtu anasikika
akiongea kwenye video hiyo.
Zaidi ya wahamiaji 181,000 waliwasili Italia
kwa mashua mwaka 2016 wengi kutoka nchi
za Afrika ambalo ni ongezeko la karibu
asilimia 18 ikilinganishwa na mwaka 2015.

Related Posts:

  • Bunge la Uingereza lakosoa EU Kamati ya bunge la Uingereza imekosoa operesheni ya Muungano wa Ulaya kukabiliana na biashara ya kusafirisha watu kimagendo katika bahari ya Mediterranean. Kamati hiyo imesema kuwa meli za muungano huo zimewaokoa maelfu… Read More
  • Twitter ya mtumbua jipu Mwanamuziki Mwanamuziki wa mtindo wa Rap Azealia Banks amepigwa marufuku na mtandao wa Twitter. Nyota huyo wa 212 amezuiliwa kuingia katika mtandao huo kufuatia hatua yake ya kutumia mtandao huo kumtusi msanii Zayn Malik. Ameshtumiwa k… Read More
  • Papa aruhusu mjadala wa wanawake mashemasiPapa aliahidi kubuni tume kutafiti na kujadili uwezekano huo wa kuwezesha wanawake kuhudumu katika ngazi hiyo ambayo ni daraja moja tu chini ya makasisi. Wanahistoria wanasema zamani wanawake walihudumu kama mashemasi. M… Read More
  • Mwanamke mkongwe zaidi duniani afariki New York Mwanamke aliyetambuliwa kuwa mkongwe zaidi duniani ameaga dunia akitibiwa jijini New York, Marekani, madaktari wamesema. Susannah Mushatt Jones, amefariki akiwa na umri wa miaka 116 Alizaliwa eneo la mashambani jimbo la Al… Read More
  • Korea Kaskazini 'inaihami DR Congo'Ripoti ya siri ya wataalamu wa Umoja wa mataifa ilioonekana a shirika la habari la Reuters inaarifu kuwa maafisa kadhaa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo wamesema kuwa Korea kasakzini imewapatia wanajeshi na polisi ba… Read More