Recent Posts

PropellerAds

Saturday, January 14, 2017

Magufuli ayatahadharisha magazeti kuhusu uchochezi Tanzania

Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli, ameyaonya magazeti mawili ambayo amesema yanaandika habari za uchochezi na kupotosha wananchi.
Amesema hatua ya magazeti hayo inahatarisha amani nchini humo.
Rais Magufuli ametoa onyo hilo wakati akikagua na kufungua kiwanda cha Jambo cha kuzalisha vinywaji baridi mkoani Shinyanga kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ikulu, kiongozi huyo amesema serikali haitayavumilia magazeti hayo mawili akisema yanaweza kuhatarisha amani ya nchi kama ilivyotokea katika nchini jirani ya Rwanda na kupelekea mauaji ya kimbari nchini humo.
''Serikali ya kutumbua majipu haiwezi kuacha kutumbua magazeti yanayofanya mambo ya uchochezi hatuwezi kuiacha Tanzania ikawa dampo la eneo la kuweka maneno ya uchochezi chini ya utawala wangu," alisema Dkt Magufuli.
Magufuli atia saini sheria ya wanahabari
Magufuli: Mwacheni Kikwete apumzike
Mwanzilishi wa Jamii Forums ashtakiwa Dar es Salaam
"Hilo halitakuwepo kuna magazeti mawili tu kila ukisoma wao ni kuchochea tu ikizungumzwa habari hii wao wanageuza hii nasema na nataka wanisikie siku zao zimeshafika kama wanasikia wasikie wasiposikia wasisikie lakini magazeti mengine na vyombo vyote vingine vinatoa uchambuzi mzuri sana''.
Rais Magufuli amekuwa akikosolewa na baadhi ya wadau kwa tuhuma kwamba anakandamiza uhuru wa vyombo vya habari.
Baraza la Habari nchini Tanzania tayari limewasilisha kesi mahakamani kupinga Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari iliyopitishwa na bunge la nchi hiyo Novemba mwaka jana na siku chache baadaye ikatiwa saini na Rais Magufuli.
Mwishoni mwa mwaka jana, mwanzilishi wa mtandao wa Jamii Forums Maxence Melo alikamatwa na kushtakiwa kwa kukataa kufichua maelezo kuhusu watu wanaochangia kwenye mtandao huo.
Aliachiliwa huru baada ya kuzuiliwa kwa takriban wiki moja.

Related Posts:

  • Why You Have That Thorn I have a “thorn in the flesh.” I don’t like it. I often wish I didn’t have it. At times I am exasperated by it. It makes almost everything harder, daily dogging me as I carry out my family, vocation, and ministry responsib… Read More
  • God Is at Work in Your Unremarkable Days I’m reading in Genesis now, as I often do at the beginning of the year, once again on a one-year journey through the greatest, most influential book ever published in human history. I’m in my fiftieth year, and having spen… Read More
  • Awkward Is Better Than Silent The Citadel of Erbil in Northern Iraq sits high in the center of town. It’s an UNESCO site filled with ancient history. “The oldest continuous living community on the planet,” reads the marker on the gate. One day friends… Read More
  • The Dangerous ‘Well Done’ It is sometimes good, and often dangerous, to be praised by other people. We know praise from others is sometimes good because the writer of Proverbs says, “a woman who fears the Lord is to be praised” (Proverbs 31:30). T… Read More
  • Loving Our Enemies: A Divine Task It was the last day of school before the Christmas holidays when 10-year-old Chris Carrier was walking home from school. He was just two houses away from his home when an older-looking man approached him. The man introduce… Read More