Recent Posts

PropellerAds

Sunday, January 22, 2017

Trump ashambulia vyombo vya habari kufuatia picha za kuapishwa kwake

Siku moja baada ya Rais wa Marekani
Donald Trump kuchukua hatamu ya uongozi
wa taifa hilo, amelaamu baadhi ya vyombo
vya habari kwa kueneza taarifa za uongo juu
ya idadi ya watu waliyohudhuria sherehe ya
kuapishwa kwake.
Trump amesema zaidi ya watu milioni moja
walihuthuria sherehe hiyo.
Msemaji wa White House, Sean
Spicer,amesema vyombo hivyo vya habari
vinaendesha kampeni ya kugawanya watu
kwa kuangazia habari ambazo hazina msingi
wowote.
Hata hivyo kanda za video za matangazo ya
moja kwa moja wakati wa hafla hiyo
hazikunasa umati mkubwa wa watu.
Picha zinaonekana zikionyesha watu wengi
waliohudhuria shereha ya kupishwa kwa rais
Barack Obama mwaka 2009.
Trump aanza kufanyia mabadiliko sheria
za Obama
Maandamano yashuhudiwa ulimwenguni
Bwana Trumpo hakuzungumzia maandamano
wakati alitembelea makao makuu ya CIA
jimbo la Virginia siku ya Jumamosi, lakini
badala yake alishambulia vyombo vya
habari.
Bwana Trump alisema kuwa video na picha
wakati wa kuapishwa kwake zilionyesha
taarifa ziziso za ukweli.
"Walionekana kama watu milioni 1.5 siku
nya Ijumaa, alisema Trump, na kuzua ripoti
za vyombo vya habari kuwa walikuwa wati
chini ya 250,000.
Rais huyo mpya aliwataja waandishi wa
habari kuwa watu waongo zaidi duniani.