Waziri wa ulinzi wa Marekani Ashton Carter, amesema shambulizi la anga lililowalenga wapiganaji wa kiislamu nchini Libya limeuwa zaidi ya washukiwa nane.
Shambulizi hilo lilitekelezwa na mpiga shaba wa umbali mrefu wa Marekani likielekezwa katika vikundi viwili vya wapiganaji wa kiislamu siku ya Jumatano, katika eneo la jangwa Kusini Magharibi mwa Pwani ya Mji wa Sirte.
Bwana Carter amesema wengi wa waliofariki inaaminika kuwa walikuwa washambuliaji wa mara kwa mara huko Ulaya.
Maafisa wamearifu kuwa shambulizi hilo la anga, lilitekelezwa kwa ushirikiano na serikali ya Libya chini ya Mkataba wa Kitaifa wa Tripoli.
Idadi ya waliofariki kutokana na mafuriko nchini Kenya inakaribia 200
-
Idadi ya watu ambao wamepoteza maisha kutokana na mafuriko nchini Kenya
imeongezeka hadi 188, wizara ya mambo ya ndani ilisema Alhamisi, huku nchi
hiyo i...
15 minutes ago