Waziri wa ulinzi wa Marekani Ashton Carter, amesema shambulizi la anga lililowalenga wapiganaji wa kiislamu nchini Libya limeuwa zaidi ya washukiwa nane.
Shambulizi hilo lilitekelezwa na mpiga shaba wa umbali mrefu wa Marekani likielekezwa katika vikundi viwili vya wapiganaji wa kiislamu siku ya Jumatano, katika eneo la jangwa Kusini Magharibi mwa Pwani ya Mji wa Sirte.
Bwana Carter amesema wengi wa waliofariki inaaminika kuwa walikuwa washambuliaji wa mara kwa mara huko Ulaya.
Maafisa wamearifu kuwa shambulizi hilo la anga, lilitekelezwa kwa ushirikiano na serikali ya Libya chini ya Mkataba wa Kitaifa wa Tripoli.
Wanafunzi Kapeta,Kiwira warithishwa ari ya utunzaji mazingira
-
Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), kwa kushirikiana na Shirika la
Utangazaji la Tanzania (TBC), wameendesha zoezi la upandaji miti katika
Shule ya msi...
9 hours ago