Recent Posts

PropellerAds

Friday, January 6, 2017

Wasichana 800 wakeketwa kaskazini mwa Tanzania

Wasichana zaidi ya 800 walikeketwa kaskazini mwa Tanzania mwezi uliopita, mkuu wa wilaya ya Tarime Glorious Luoga amesema.
Hilo lilifanyika ingawa polisi wamekuwa wakikabiliana na utamaduni huo.
Wanawake 12 wanaotuhumiwa kuhusika katika kuwakeketa wasichana hao wamekamatwa na maafisa wa polisi, mkuu huyo wa wilaya amesema.
"Operesheni ya polisi bado inaendelea. Hatutatulia hadi wote waliohusika wakamatwe na kushtakiwa," Luoga aliambia wanahabari.
Eneo la Tarime, wasichana hukeketwa wakiwa na umri wa kati ya miaka 12 na 17.
Inakadiriwa kwamba nchini Tanzania, wasichana na wanawake 7.9 milioni wamekeketwa.
Misri imepitisha sheria kali dhidi ya Ukeketaji
Wasichana wa shule wakimbia tohara Kenya
Novemba, kabla ya kuanza kwa msimu wa ukeketaji Tarime, Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Tarime, Thomas Mapuli alikuwa ametangaza kwamba polisi wamejiandaa kuwakamata mangariba wote ambao wangejaribu kukeketa watoto wa kike.
"Tumejipanga vizuri na hatutakuwa na huruma kwa atakayekutwa anatenda kosa la ukeketaji," alisema Bw Mapuli.
Wasichana takriban 140 milioni wamekeketwa maeneo ya Afrika, Mashariki ya Kati na Bara Asia.
Jamii zinazotekeleza utamaduni huu huutazama kama njia ya kuwatakasa wasichana na kuwaandaa kwa maisha ya ndoa.
Lakini utamaduni huo husababisha matatizo mengi ya kiafya.
Wengi hufariki wakikeketwa na baadaye wengi hukabiliwa na matatizo sana wanapojifungua.

Related Posts:

  • Thoughts for the Next Generation of Leaders  Last week Athletes in Action launched a NextGen Leadership initiative. Nearly two years in the planning, we had 19 staff members and 19 coaches from the business world taking part. It was a spectacular launch to th… Read More
  • Paris yakumbwa na Mafuriko Mto Seine ulioko mjini Paris, Ufaransa, umejaa na kufikia kima cha juu zaidi kuwahi kutokea kwa zaidi ya miaka 30 iliyopita. Maji yamefurika hadi kwenye barabara na kulazimisha makavazi kadhaa na maeneo ya makaburi kufungwa… Read More
  • UM kupeleka misaada zaidi nchini Syria Maafisa wa kibalozi jijini New York wanasema kuwa hiyo kesho Umoja wa Mataifa utaomba rasmi Serikali ya Syria kuruhusu kudondosha vyakula na madawa katika maeneo wanakoishi wananchi walio katika hatari ya kufa kutokana n… Read More
  • Bondia Muhammad Ali alazwa hospitalini Bingwa wa dunia wa uzani wa juu wa zamani Muhammad Ali amelazwa hospitalini kufuatia maambikizi ya mapafu. Bondia huyo nyota mwenye umri wa miaka 74 aliyekonga nyoyo za wapenzi wa ndondi kote duniani anasemekana kuwa kati… Read More
  • Waliokuwa maafisa wa Fifa walijipatia $80m Mawakili wa FIFA wasema washukiwa wakuu wa madai ya ufisadi ambao hadi hivi majuzi walikuwa wakiliongoza shirikisho hilo la kandanda duniani walijilimbikizia nyongeza za mishahara na marupurupu mengineyo ambayo yamejumui… Read More