Waziri Mkuu wa Mauritius Anerood Jugnauth
anasema anaoandoka madarakani na
kumkabidhi mwanawe Pavind madaraka.
Waziri huyo mkuu mwenye umri wa miaka
82 alichukua wadhifa kwanza mwaka 1982.
Katika tangazo kwa njia ta runinga bwana
Jugnauth anasema anajiuzulu ili kutoka
nafasi kwa kiongozi mwenye umri mdogo
na mwenye nguvu.
Mwanawe kwa sasa ni waziri wa fedha.
Vyama vya upinzani vimekosoa hatua hiyo
lakini hakuna kile vitafanya kuzuia hatua
hiyo.
Jugnauth ni mkuu wa chama kikubwa ziadi
katika muungano unaoongoza.
Mauritius, nchi iliyo habari Hindi ni koloni ya
zamani ya Uingereza. Atakabidhi mwanawe
madaraka Jumatatu asubuhi.
Blinken atoa wito kwa Hamas kukubaliana na mapatano ya kuwasaidia Wagaza
-
Mwanadiplomasia mkuu wa Marekani Antony Blinken amewataka Hamas kukubali
mpango wa kusitisha mapigano Gaza licha ya onyo la Israel kwamba jeshi
litaendel...
26 minutes ago