Recent Posts

PropellerAds

Thursday, January 19, 2017

Donald Trump ataapishwa saa ngapi kuwa rais Marekani?

Mshindi wa uchaguzi mkuu wa mwezi Novemba Donald Trump anatarajiwa kuapishwa kuwa rais wa 45 wa Marekani Ijumaa tarehe 20 Januari, 2017.
Bw Trump wa chama cha Republican anatarajiwa kuapishwa mbele ya watu 750,000 mbele ya majengo makuu ya bunge la Marekani, Capitol Building, Washington D.C.
Kisheria, rais anafaa kuapishwa kabla ya saa sita mchana saa za Amerika Mashariki ambazo Afrika Mashariki ni saa mbili usiku.
Hii hapa ni ratiba fupi ya matukio yanayotarajiwa siku hiyo.
Saa 17:30 (Saa za Afrika Mashariki) Wanamuziki walioalikwa wataanza kutumbuiza.
19:30 Hotuba za kufungua sherehe zitaanza kutolewa.
20:00 Muda mfupi kabla ya saa Mbili Afrika Mashariki Donald Trump atalishwa kiapo cha kuwa rais wa Marekani na Jaji wa Mahakama ya Juu John Roberts.
Baadaye, kutakuwa na msafara baada ya sherehe ya kuapishwa ambao utaanza katika vidato vya jumba la Capitol Building kuelekea ikulu ya White House kupitia barabara maarufu ya Pennsylvania Avenue.
Bw Trump na mkewe Melania baadaye watacheza densi katika matamasha matatu, mawili katika ukumbi wa mikutano wa Walter E Washington na jingine katika ukumbi wa Jengo la Makumbusho ya Taifa.
Clinton kushuhudia Trump akiapishwa

Clinton na mumewe na Bush na mkewe walihudhuria sherehe ya kuapishwa kwa Barack Obama mwaka 2009.
Siku moja baada ya kuapishwa kwa Bw Trump, wanawake takriban 200,000 wanatarajiwa kuandamana Washington DC na miji mingine kumpinga Bw Donald Trump.
Donald Trump kulipwa $1 kila mwaka
Watakaoumia na watakaofaidi chini ya Trump Marekani
Hillary Clinton na mumewe Bill wamethibitisha kwamba watahudhuria sherehe hiyo, sawa na George W Bush na mkewe Laura.
Wamesema wanataka "kushuhudia kukabidhiwa madaraka kwa rasi mwingine kwa njia ya amani."
Rais mwingine wa zamani Jimmy Carter atahudhuria pia, lakini George HW Bush, 92, na mkewe Barbara hawataweza kwa sababu za kiafya.