Recent Posts

PropellerAds

Sunday, January 29, 2017

PICHA: NDOA YA BEI RAHISI KUFANYIKA DUNIAN

Vijana wawili wapenzi ambao stori yao
kuhusu ndoa ya bei rahisi waliyofunga
ilizua hisia za watu wengi kwenye
mitandao ya kijamii, sasa wameahidiwa
kulipiwa gharama zote za mapumziko
baanda ya ndoa (honeymoon).
Wilson Mutara (26) na Ann Wambui (24)
kutoka nchini Kenya inaripotiwa kuwa
walifunga ndoa kwa gharama ya Ksh 100
ambayo ni sawa na TZS 2,147 ambapo
gharama hizo zilikuwa kwa ajili ya
kununua pete tu.
Ndoa hiyo iliyotajwa kuwa ya bei rahisi
kuwahi kutokea nchini humo haikua na
sherehe baada ya wawili hao kutoka
kanisani na walivalia fulana walipokwenda
kufunga ndoa.
“Tulikwenda nyumbani tukapika ugali na
sukuma wiki, tukala na tukalala. Hakuna kitu
cha kipekee tulichokifanya katika mapumziko
(honeymoon) yetu” alisema Mutura.
Padri aliyefungisha ndoa hiyo alichapisha
habari hiyo na ndipo mwakilishi wa
Kampuni ya Utalii ya Bonfire Adventure
alipokutana na wanandoa hao.
Kampuni hiyo ndiyo ilijitolea kudhamini
mapumziko ya wawili hao baada ya
kufunga ndoa.

Related Posts:

  • Trump alegeza msimamo kuhusu WaislamuMgombea Urais wa Republican anaonekana kulegeza msimamo kuhusiana na pendekezo lake tata la kuwazuia Waislamu kuingia Marekani. Katika mahojiano na kituo cha television cha Fox News, Donald Trump akijibu kauli ya meya mpya wa… Read More
  • Besigye akamatwa kwa 'kujiapisha' UgandaTaharuki imetanda nchini Uganda baada ya kiongozi wa upinzani Dr Kizza Besigye, ''kujiapishwa kama rais'' siku moja tu kabla ya kuapishwa rasmi kwa rais Yoweri Museveni . Haijulikani ni vipi Dr Kiiza Besigye alikwepa kizuizi … Read More
  • MAGAZETI YA LEO MEI 12 Read More
  • Kongamano la uchumi kufanyika Rwanda Kongamano la 26 la uchumi duniani linaanza leo mjini Kigali Rwanda. Hii ni mara ya kwanza kongamano hilo kuandaliwa Rwanda na mara yake ya pili kufanyika afrika mashariki. Kongamano hilo litakalowaleta pamoja marais wa mat… Read More
  • Orodha ya Mataifa fisadi zaidi Afrika MasharikiBaada ya waziri mkuu wa Uingereza David Cameron kunaswa na kamera akiidunisha Nigeria kuwa mafisadi wakuu kote duniani BBC imeamua kuangazia kwa umakini ikiwa matamshi hayo ni ya kweli. Je Nigeria imeorodheshwa katika nafasi … Read More