Recent Posts

PropellerAds

Thursday, January 26, 2017

Mwanaume apotea njia na kuendesha baiskeli siku 30

Mwanamume mmoja nchini China ambaye
alikuwa na matumaini ya kuendesha baiskeli
hadi nyumbani kwao kusherehekea mwaka
mpya, aligundua baada ya siku 30 kuwa
alikuwa amepotea njia.
Mwanamume huyo alikuwa na matumaini ya
kuwasil nyumbani kwao huko Qiqihar mkoa
wa Heilongjian baada ya kuanzia safari yake
huk Rizhao umbali wa kilomita 1,700.
Lakini alisimamishwa na polisi wa trafiki
akiwa amepotea umbali wa kilomita 500
katika mkoa wa Anhui.
Wakati waligundua, polisi walimlipia tikiti ya
treni ili arudi nyumbani.
Ripoti zinasema kwa mwanamume huyo
alikuwa akilala maduka ya intaneti kwa
sababu hakuwa na pesa.
Mwanamume huyo hakuwa na uwezo wa
kusoma ramani na hivyo alikuwa akitegemea
watu kumuelekeza.
Polisi walimsimamisha kwa sababu alikuwa
akitumia barabara ambayo baiskeli
haziruhisiwi kuitumia.
Baada ya kugundua makosa yake, polisi na
watu wote waliokuwa kituoni ambapo
alisimama walichanga pesa na kumnunulia
tikiti ili asafiri nyumbani.

Related Posts:

  • Everton yamfuta kazi kocha wake Klabu ya Everton imempiga kalamu mkufunzi wake Roberto Martinez baada ya kuifunza klabu hiyo kwa miaka mitatu. Kilabu hiyo ya Martinez ilio katika nafasi ya 12 katika jedwali li ligi ya Uingereza ilishindwa 3-1 na mabingw… Read More
  • Rais Yoweri Museveni aapishwaYoweri Museveni leo ametawazwa rasmi kuwa Rais mpya wa Uganda kwa muhula wa tano mfululizo.Tayari Rais Museveni amekwisha tawala miaka 30. Kutawazwa kwake leo, ambako kunashuhudiwa na viongozi wa mataifa 14 kutoka Afrika na w… Read More
  • Trump alegeza msimamo kuhusu WaislamuMgombea Urais wa Republican anaonekana kulegeza msimamo kuhusiana na pendekezo lake tata la kuwazuia Waislamu kuingia Marekani. Katika mahojiano na kituo cha television cha Fox News, Donald Trump akijibu kauli ya meya mpya wa… Read More
  • Besigye akamatwa kwa 'kujiapisha' UgandaTaharuki imetanda nchini Uganda baada ya kiongozi wa upinzani Dr Kizza Besigye, ''kujiapishwa kama rais'' siku moja tu kabla ya kuapishwa rasmi kwa rais Yoweri Museveni . Haijulikani ni vipi Dr Kiiza Besigye alikwepa kizuizi … Read More
  • Orodha ya Mataifa fisadi zaidi Afrika MasharikiBaada ya waziri mkuu wa Uingereza David Cameron kunaswa na kamera akiidunisha Nigeria kuwa mafisadi wakuu kote duniani BBC imeamua kuangazia kwa umakini ikiwa matamshi hayo ni ya kweli. Je Nigeria imeorodheshwa katika nafasi … Read More