Recent Posts

PropellerAds

Sunday, January 22, 2017

Watu 16 wafariki ajali ya basi la shule Italia

Basi lililokuwa limewabeba watoto wa shule
limegonga nguzo ya umemena kushika moto
kaskazini mwa Italia.
Maafisa wa huduma za dharura wanasema
watu 16 wamefariki.
Basi hilo lilikuwa limewabeba wanafunzi
kutoka Hungary na liligonga nguzo ya
umeme lilipokuwa linatoka kwenye barabara
kuu karibu na mji wa Verona Ijumaa usiku.
Maafisa wa huduma za dharura wa Italia
wamesema kwenye Twitter kwamba watu 39
wamejeruhiwa.
Basi hilo lilikuwa safarini kuelekea Budapest
kutoka Ufaransa, ambapo wanafunzi hao
walikuwa wameenda kwa likizo milimani.
Shirika la habari la Italia Ansa limesema
wanafunzi kadha, wengi wavulana,
walirushwa nje basi hilo lilipogonga nguzo
hiyo.
Wengine walikuwa wamekwama ndani ya
basi liliposhika moto, Ansa imeripoti.
Idadi ya waliofariki haitarajiwi kuongezeka,
maafisa wa huduma za dharura wanasema.

Related Posts:

  • bandari ya Dar es salam kupanuliwa kwa gharama ya $ 305.Tanzania inasema kuwa itapokea dola milioni 305 kama mkopo kutoka kwa Benki ya Dunia, kugharamia upanuzi wa bandari kwenye mji wa Dar es Salaam. Bandari hiyo ndiyo inaunganisha mataifa ya Afrika ambayo hayapakani na bahari ya… Read More
  • JE? NI KICHWA GANI UNACHOTUMIA KUFANYA MAAMUZI..? Na Mwl John C Ntogwisangu_ Mwanaume ana Vichwa viwili, Kimoja kipo juu na kingine kipo chini. Vichwa Vyote vina Kazi yake na umuhimu wake Katika Mwili, hakuna kilicho bora kuliko kingine. Vichwa hivi mara nyingi hupingana … Read More
  • Ajiuzulu baada ya papa kumtaka asambaze kondomuKiongozi wa kanisa katoliki anayewasaidia raia wa Malta amejiuzulu kufuatia mgogoro na Vatican kuhusu mpango wa kusambaza mipira ya kondomu kulingana na kanisa hilo. Mathew Festing mwenye umri wa miaka 67 alijiuzulu baada ya … Read More
  • Al-Shabab washambulia hoteli Mogadishu Wanamgambo wanaoshukiwa kuwawanachama wa al-Shabab wameshambuliahoteli moja katika mji mkuu wa SomaliaMogadishu.Watu hao wenye silaha wameingia kwenyehoteli hiyo baada ya kulipuliwa kwa mabomumawili kwenye lango la kuingia k… Read More
  • 7 Tips for Network Marketing Successmarketing (also known as direct sales or multilevel marketing) is all about-- housewives buying and selling Tupperware while gossiping and eating finger sandwiches, or a high-pressure salesperson trying to convince you how ea… Read More