Recent Posts

PropellerAds

Saturday, April 30, 2016

Newcastle yanusurika,Sunderland yapata sare

Klabu ya Newcastle imaimarisha matumaini yake ya kusalia katika ligi kuu ya Uingereza kufuatia bao la Andros Townsend na penalti iliopanguliwa na kipa wa kilabu hiyo dhidi ya Crystal palace. Huku Norwich ikicheza dhidi ya Arsenal na Sunderland kutoka sare na Stoke,Newcastle sasa imepanda hadi nafasi ya 17 na kuondoka katika eneo la kushushwa daraja. Towsend aliipatia...

Uwindaji haramu: Kenya yachoma pembe za ndovu

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amezichoma pembe za ndovu katika juhudi za kuonyesha taifa lake kuhusu umuhimu wa kuwahifadhi ndovu. Zaidi ya tani 100 za pembe za ndovu zilikusanywa katika mbuga ya wanyama ya Nairobi ambapo zinatarajiwa kuchomeka kwa siku kadhaa. Pembe hizo zinawakilisha karibia pembe zote zilizopatikana na serikali zikidaiwa kutoka kwa takriban ndovu 6,700. Hatahivyo...

Uhuru ataka mmiliki wa jumba la maafa kukamatwa

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametaka kukamatwa kwa mmiliki wa nyumba ilioanguka mjini Nairobi na kuwaua watu saba. Kenyatta aliyezuru mkasa wa tukio hilo pia amewataka wakaazi wa nyumba zilizopo karibu na eneo hilo kuondoka wa kuwa nyumba hizo zimethibitishwa kutokuwa salama. Maafisa wa Kaunti ya Nairobi wamethbitisha kuwa nyumba hiyo ilikuwa imeorodheshwa miongoni mwa...

Msikiti waporomoka na kuwaua watu 15 Mogadishu

Msikiti uliokuwa ukikarabatiwa umeporomoka nchini Somalia na kuwaua watu 15 na kuwajeruhi wengine 40. Kisa hicho kilitokea katika msikiti mmoja wa mjini Mogadishu wakati wa ibada ya Ijumaa. Hatahivyo maelezo yalitolewa siku ya Jumamosi.Mamia ya watu walidaiwa kuwa ndani ya msikiti huo wakati ulipoporomoka na wengine wanaaminika kuwa chini ya vifusi vya jengo hilo la ibada. Muhandisi...

Ada ya kupiga simu Ulaya yashuka kwa 75%

Ada ya kupiga simu kupitia mitandao mingine katika muungano wa bara Ulaya imeshuka kwa kiwango kikubwa, ikiwa ni hatua ya mwisho kabla ya ada hiyo kuondolewa kabisa kwa raia wa bara Ulaya mwaka ujao. Ada hiyo huwa haiwapendezi raia wengi wa bara hilo wanaosafiri kwa shughuli za kibiashara na burudani. Tume ya muungano huo inasema ada hiyo imeshuka kwa asilimia 75. Serikali...

Urusi na Marekani zalaumiana kuhusu uchokozi wa ndege

Urusi inasema kuwa ilikuwa na haki kuikabili ndege moja ya Marekani katika bahari ya Baltic siku ya Ijumaa. Hatua hiyo inajiri baada ya Marekani kusema kuwa ndege ya kijeshi ya Urusi ilizua hofu ya kiusalama baada ya kuzunguka karibu na ndege yake. Urusi inasema kuwa ndege hiyo ya Marekani ilikuwa imezima kifaa chake cha kurusha ishara zake ambazo husaidia wengine kuitambua. Ni...

Waandamana dhidi ya chama chenye sera zinazopinga Uislamu

olisi nchini Ujerumani wamewazuilia mamia ya waandamanaji wanaopinga chama cha mrengo wa kulia cha AFD. Zaidi ya maafisa 1000 wametumwa katika eneo la mkutano wa chama hicho katika mji wa Stuttgart kutoa ulinzi. Polisi wametumia maji ya pilipili kuwatawanya waandamanaji waliobeba vijiti na vyuma, na kuchoma moto tairi kwenye kiingilio cha eneo la mkutano wa chama hicho,...

Maandamano yachelewesha hotuba ya Trump

Maafisa wa polisi wa kutuliza ghasia nchini Marekani, wamewaondoa maelfu ya waandamanaji walioshiriki katika maandamano makubwa nje ya eneo la mkutano wa chama cha Republican, ambapo mgombea wa tiketi ya urais wa chama hicho Donald Trump alikuwa akihutubia. Mgombea huyo aliingia katika eneo la mkutano chini ya ulinzi wa maafisa wanaomlinda rais wa Marekani maarufu kama...

Jumba lililoporomoka lawaua watu 7 Nairobi

Polisi katika mji mkuu wa Kenya Nairobi wanasema kuwa takriban watu saba waliuawa wakati nyumba moja ilipoanguka katika mtaa mmoja mjini humo. Waokoaji wanaendelea kutafuta watu wanaohofiwa kukwama ndani ya vifusi vya jengo hilo la ghorofa sita kufuatia mvua kali inayoendelea kunyesha ambayo imesababisha mafuriko. Takriban watu 120 wameokolewa kufikia sasa katika mtaa...

MAGAZETI YA LEO APRILI 30

...

Friday, April 29, 2016

Je huu ni mji mkongwe kutoka Tanzania?

Mpiga mbizi mmoja anaamini amegundua kile ambacho huenda ni mji mkongwe kutoka pwani ya Tanzania ambao ulimezwa na bahari, kwa mujibu wa taarifa kutoka gazeti la nchini humo Dar Post. Katika blogu yake Alan Sutton amesema alikuwa kwenye helikopta akielekea kisiwa cha Maffia wakati 'aliona muundo fulani ndani maji'. Alirudi katika sehemu hiyo na kugundua masalio yenye umbali...

Magufuli: Polisi sharti wajirekebishe

Rais wa wa Tanzania Dkt John Magufuli amelitaka jeshi la polisi nchini pamoja na ofisi ya mwendesha mashitaka kujirekebisha katika utenda kazi na kujiepusha na kashfa. Amesema taarifa zinaonesha jeshi la polisi limekuwa likihusishwa na matumizi mabaya ya fedha hali inayoongeza ukubwa wa matatizo yanayokwamisha utendaji wake wa kazi. Akiongea alipokuwa akifungua kikao...

Je, ni wakati gani mtoto huwa mtu mzima?

Jaji mmoja nchini Kenya amemwachilia huru mshukiwa mmoja ambaye alikuwa amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa kumbaka mtoto wa miaka 13. Ijapokuwa umri wa mtoto kuwa mtu mzima nchini Kenya ni miaka 18 jaji aliamuru kwamba kesi hiyo haiwezi kuwa ya ubakaji kwa kuwa mtoto huyo alijifanya kuwa mtu mzima na kwamba alikuwa akifurahia kufanya tendo la ngono na wanaume. Hatahivyo...

Compassion

Compassion Enhances: Caring Balances/Counters: Judgment, Pain The Basic Practice Compassion is a feeling deep within ourselves —a "quivering of the heart" — and it is also a way of acting — being affected by the suffering of others and moving on their behalf. Buddha and Jesus are the most well known exemplars of compassion, and it is...

Wafanyakazi hawajalipwa Nigeria

  Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari amesema ana wasiwasi mkubwa kwamba karibu theluthi mbili ya majimbo 36 nchini humo hayana uwezo wa kuwalipa waanyakazi mishahara, licha ya kupokea udhamini kutoka kwa serikali ya shirikisho. Rais Buhari amesema atajaribu kuwasilisha fedha zaidi lakini ameonya kwamba serikali kuu pia inakabiliwa na matatizo ya fedha. Ni hivi maajuzi...

Ndege ya abiria 14 yaanguka Norway

Ndege moja imeanguka karibu na mji wa Norway wa Bergen huku ikiwa na abiria 14 na kuna ripoti ya watu kuonekana katika bahari. Maafisa wa uokoaji wameviambia vyombo vya habari kwamba ndege hiyo imeharibika vibaya. Picha kutoka katika eneo la mkasa huo zinaonyesha moshi mkubwa ukifuka katika eneo lenye mwamba mkubwa. Gazeti la Norway Aftonbladet limeripoti kwamba ndege...

Serikali mpya ya umoja yaundwa Sudan Kusini

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amelivunja bunge lake na kuunda serikali ya umoja, katika harakati za kupiga jeki makubaliano ya amani yanayolenga kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vya takriban miaka miwili. Mpango huo unaowashirikisha waliokuwa waasi katika serikali ulitangazwa Alhamisi katika runinga ya taifa. Theluthi moja ya mawaziri wa bunge hilo jipya ni wanachama...

Mmarekani ahukumiwa kufungwa na kazi ngumu Korea

Raia wa Marekani amefungwa jela miaka 10 na kazi ngumu nchini Korea Kaskazini baada ya kupatikana na makosa ya kufanya ujasusi, shirika la habari la Uchina la Xinhua limeripoti. Kim Dong-chul, raia wa Marekani aliyezaliwa Korea Kusini, alikamatwa mwezi Oktoba mwaka jana. Kim aliwasilishwa kwa wanahabari mjini Pyongyang mwezi jana na akaoneshwa akikiri makosa, na kusema...

Iran yaitaka Marekani kuachilia mali

Iran imetoa wito kwa Umoja wa Mataifa kuihimiza Marekani, kuachilia mali yake yaliyoshikiliwa katika benki za Marekani, sambamba na makubaliano ya mwaka uliopita ya vikiwazo wa kinyuklia. Iran imeghadhabishwa na uamuzi wa mahakama ya juu nchini Marekani kuwa mali yake yote, yenye thamani ya dola bilioni mbili, iliyoshikiliwa nchini Marekani, ni lazima ikabidhiwe jamaa za...

Thursday, April 28, 2016

Biden afanya ziara ya ghafla Iraq

Makamu wa rais wa Marekani, Joe Biden, ameiunga mkono serikali ya Iraq iliyoko taabani, baada ya ziara yake ya ghafla, na ya kwanza nchini humo kwa kipindi cha miaka mitano. Ikulu ya White House inasema ziara hiyo ilikuwa ishara ya kuunga mkono serikali ya Iraq, kutokana na juhudi za waziri mkuu Haider al-Abad...

Watu 50 wauawa katika mashambulio Aleppo

Maafisa wa ulinzi wa raia katika mji mkuu wa Syria Aleppo, wanasema kuwa karibu watu 50 waliuwawa baada ya mashambulio ya angani yaliyotekelezwa na vikosi vya serikali, katika hospitali moja Jumatano usiku. Wafanyikazi hao, wa kundi linalojulikana kama "White Helmets" walikuwa wakichimba vifusi saa 24 baada ya mashambulizi hayo ya mabom...

UK yashauriana na Cuba

Waziri wa mambo ya kigeni wa Uingereza Philip Hammond ameshiriki kikao cha mzungumzo na mwenzake wa Cuba Bruno Rodríguez, katika ziara ya kwanza tangu mapinduzi ya mwaka 1959. Mazungumzo hayo yalijikita katika vigezo vinne muhimu: huduma za kifedha, kawi, elimu ya juu na utamadu...

Kenyatta ataka hatua madhubuti kulinda ndovu

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametoa wito wa hatua madhubuti kuchukuliwa dhidi ya biashara haramu ya pembe, kabla ya kongamano la viongozi wa bara Afrika la kujadili mikakati ya kuwalinda ndovu. Rais Kenyatta amesema kuwa ndovu wanakabiliwa na hatari ya kuangamizwa na kizazi kipya cha wawindaji haramu, waliojihami vilivo na walio na uhusiano wa kimataifa, na matokeo yake yamekuwa...

MAGAZETI YA LEO APRIL 29

...