olisi nchini Ujerumani wamewazuilia mamia ya waandamanaji wanaopinga chama cha mrengo wa kulia cha AFD.
Zaidi ya maafisa 1000 wametumwa katika eneo la mkutano wa chama hicho katika mji wa Stuttgart kutoa ulinzi.
Polisi wametumia maji ya pilipili kuwatawanya waandamanaji waliobeba
vijiti na vyuma, na kuchoma moto tairi kwenye kiingilio cha eneo la
mkutano wa chama hicho, ili kuwazuia wanachama wake.
Chama hicho kinatarajiwa kuzinduliwa upya, na kutangaza wazi kuwa kinapinga dini ya kiislamu.
Chama hicho kinapanga kupiga marufuku vazi la kidini la burqa, minara ya
misikiti ambapo mwadhini hutangaza wito wa maombi, na pia kupiga
marufuku mwito huo wa waadhini.
CCM wilaya ya mbogwe walia na tozo mazao ya chakula kwa wakulima.
-
Wananchi na Wakulima katika Halmashauri ya wilaya ya Mbogwe Mkoani Geita
wamewalalamikia viongozi wao wa kata kwa kushindwa kudhibiti Baadhi ya
watumishi...
36 minutes ago