Recent Posts

PropellerAds

Saturday, April 30, 2016

Waandamana dhidi ya chama chenye sera zinazopinga Uislamu

olisi nchini Ujerumani wamewazuilia mamia ya waandamanaji wanaopinga chama cha mrengo wa kulia cha AFD.
Zaidi ya maafisa 1000 wametumwa katika eneo la mkutano wa chama hicho katika mji wa Stuttgart kutoa ulinzi.

Polisi wametumia maji ya pilipili kuwatawanya waandamanaji waliobeba vijiti na vyuma, na kuchoma moto tairi kwenye kiingilio cha eneo la mkutano wa chama hicho, ili kuwazuia wanachama wake.
Chama hicho kinatarajiwa kuzinduliwa upya, na kutangaza wazi kuwa kinapinga dini ya kiislamu.
 Chama hicho kinapanga kupiga marufuku vazi la kidini la burqa, minara ya misikiti ambapo mwadhini hutangaza wito wa maombi, na pia kupiga marufuku mwito huo wa waadhini.