Recent Posts

PropellerAds

Monday, April 4, 2016

CUF: Hatumtambui Shein kama rais Zanzibar

Chama kikuu cha upinzani visiwani Zanzibar kimesema
hakimtambui Dkt Mohamed Ali Shein aliyetangazwa
kuwa mshindi wa uchaguzi wa marudio uliofanyika mwezi
uliopita.
Viongozi wa Chama cha Wananchi (CUF),
wakizungumza kwa mara ya kwanza tangu kufanyika kwa
uchaguzi huo ambao chama hicho kilisusia, wamesema
hawamtambui Dkt Shein kama rais wa visiwa hivyo.
“Tangu mapema, tangu Jecha (Mwenyekiti wa Tume ya
Uchaguzi Zanzibar Jecha Salim Jecha) alipofuta
uchaguzi, tulisema waziwazi kwamba haikuwa halalali.
Walipoitisha uchaguzi wa marudio, tulisema waziwazi
uchaguzi huo sisi hatuutambui na tukawataka wananchi
wasipige kura,” amesema Katibu Mkuu wa CUF Maalim
Seif Sharif Hamad.
Bw Hamad alikuwa mgombea urais wa chama hicho
katika uchaguzi uliofanyika tarehe 25 Oktoba mwaka
jana na ambao matokeo yake yalifutwa na tume.
“Kama Rais ametokana na mchakato ambao
hamkuutambua nyinyi tangu mwanzo, sasa leo kuja
kusema hatumtambui kwa nini iwe ni haramu?
Hatumtambui.”
Chama hicho kimesema kitatumia njia za kidemkrasia
kulalamika dhidi ya Dkt Shein na serikali yake.
Tanzania yasikitika kunyimwa pesa za MCC
Mabalozi wakosoa uchaguzi wa Zanzibar
Aidha, kimeiomba jamii ya kimataifa kuwawekea vikwazo
watu binafsi waliofanikisha uchaguzi huo wa marudio
ambao chama hicho kimesema ulikuwa “uongozi
haramu”.
Wiki iliyopita, Shirika la Changamoto za Milenia la
Marekani (MCC) lilisitisha ufadhili wa $472milioni
kwa Tanzania likilalamikia uchaguzi visiwani Zanzibar na
utekelezwaji wa Sheria ya Uhalifu wa Mtandao.
Pesa hizo zilikuwa za kutumiwa katika miradi ya
kusambaza umeme.

Related Posts:

  • Ask God to Rebuild What Is Broken The last year has been one of the most confusing, troubling, and heartbreaking for many Christians in America, especially for younger believers. It has felt at times like every new day has brought its own dark wave of re… Read More
  • Watch Where You Walk in 2018 The Christian life is not a sprint. It is a journey of ten million steps. Day after day, and year after year, we put one foot in front of the other as we flee the wreckage of our sin and follow Jesus on the path of life… Read More
  • He Will Restore Your Soul King David wrote Psalm 22 and Psalm 23, but if we weren’t told that, we might not believe it. These two ancient songs of the faith are about as different as they could be. The first few verses of each psalm capture its t… Read More
  • Losing Your Life to Find It "Whosoever seeks to save his live will lose it, and whosoever loses his life for my sake will find it." By kenedy Jagaji       These words of Jesus are familiar … Read More
  • Taste the Goodness of GodLike newborn babies — so he’s picking up on “You just got born.” So 1 Peter 2:2–3, Like newborn babies, desire the pure milk — meaning the word, not distinguishing it from meat at all. That’s not what’s going on here. This… Read More