Ada ya kupiga simu kupitia mitandao mingine katika
muungano wa bara Ulaya imeshuka kwa kiwango
kikubwa, ikiwa ni hatua ya mwisho kabla ya ada hiyo
kuondolewa kabisa kwa raia wa bara Ulaya mwaka
ujao.
Ada hiyo huwa haiwapendezi raia wengi wa bara hilo
wanaosafiri kwa shughuli za kibiashara na burudani.
Tume ya muungano huo inasema ada hiyo imeshuka
kwa asilimia 75.
Serikali imesema kuwa wale wanaopiga simu ,kupakua
data ama kutuma ujumbe watahifadhi mamilioni ya
pauni kwa ada kufuatia mabadiliko hayo.
Mamilioni ya Waingereza hutumia pauni milioni 350 kila
mwaka kutokana na ada hizo za kupiga simu miongoni
mwa mataifa ya bara hilo,alisema waziri wa uchumi wa
kidijitali Ed Vaizey.
CCM wilaya ya mbogwe walia na tozo mazao ya chakula kwa wakulima.
-
Wananchi na Wakulima katika Halmashauri ya wilaya ya Mbogwe Mkoani Geita
wamewalalamikia viongozi wao wa kata kwa kushindwa kudhibiti Baadhi ya
watumishi...
1 hour ago