Recent Posts

PropellerAds

Sunday, April 3, 2016

Bunge kujadili hoja ya kumn'goa Zuma Jumanne

Bunge la Afrika kusini litajadili hoja ya kumng'oa rais
Jacob Zuma madarakani siku ya Jumanne.
Spika wa bunge la Afrika Kusini ametoa taarifa hiyo
baada ya shinikizo kutoka kwa vyama vya upinzani
vikiongozwa na kile cha Economic Freedom Fighters
(EFF) kinachoongozwa na Julius Malema.
Spika Baleka Mbete, amesema wakati umewadia wa
kujadili wito wa kumfuta kazi rais Zuma kufuatia tuhuma
za ufisadi ubadhirifu wa mali ya umma na matumizi
mabaya ya madaraka yake.
Vyama vya upinzani vilikuwa vimemtaka ajiuzulu baada
ya kupatikana na hatia ya kutumia madaraka yake
vibaya kwa kuidhinisha ukarabati wa makazi yake licha
ya kushauriwa asifanye hivyo.
Siku ya Alhamisi, mahakama kuu ya nchi, ilisema kuwa
rais amekwenda kinyume na katiba, katika kashfa ya
mamilioni ya dola, yaliyotumiwa kukarabati nyumba yake
ya binafsi.
Upinzani uliwasilisha kesi mahakamani baada ya bwana
Zuma kupuuza uamuzi wa mwaka 2014 kuwa alinufaika
kutokana na ukarabati wa nyumba yake na kwamba
alistahili kulipa pesa zilizotumiwa.
Mahakama ilisema wizara ya fedha itatambua ni kiasi
gani cha pesa kilichotumiwa na kwamba Zuma
atatakikana kuzirejesha.
Rais Jacob Zuma alikubali uamuzi wa mahakama ya
kikatiba uliompata na hatia na akaapa kulipia ukarabati
uliofanyiwa makao hayo ya Nkandla kama ilivyoamua
mahakama.

Related Posts:

  • Far Worse Than Being Caught Fighting Sin with Fear There is something more dreadful in this world than when God makes us miserable because of our sin: when God uses more sin to make us miserable because of our sin. This is more dreadful because misery may be a wake-up ca… Read More
  • God Heals by Humbling “I have seen his ways, but I will heal him; I will lead him and restore comfort to him and his mourners, creating the fruit of the lips. Peace, peace, to the far and to the near,” says the Lord, “and I will heal him.” (I… Read More
  • Love the One You’re With It can be really hard to love the church. Every Christian, who’s been one for very long, knows this. The earthly church has always been a motley crew. It’s never been ideal. The New Testament exists because churches, to… Read More
  • Love and Respect Basics for Marriage Scripture teaches us that Christians should honor or respect all men (1 Peter 2:17). Every human being bears the image of God, and so, of course, we are called on to respect and honor that. And of course, Scripture also t… Read More
  • Let’s (Not) Talk About Sex, Baby We all know boundaries are vital for healthy relationships, and especially for dating relationships. Even if you’ve been prone to cross the lines you’ve drawn in the past, you can admit that lines need to be drawn between… Read More