Recent Posts

PropellerAds

Friday, April 15, 2016

Sudan Kusini kujiunga na Afrika Mashariki

MagufuliRais wa Sudan Kusini Salva Kiir anatarajiwa kutia saini mkataba wa kuiingiza rasmi nchi hiyo kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Rais Kiir atatia saini mkataba huo jijini Dar es Salaam mbele ya mwenyeji wake, Rais wa Tanzania John Magufuli, ambaye kwa sasa ndiye mwenyekiti wa jumuiya hiyo.
Viongozi wa nchi za jumuiya hiyo waliidhinisha kukubaliwa kwa Sudan Kusini kujiunga na jumuiya hiyo kwenye mkutano mkuu uliofanyika mjini Arusha mwezi uliopita.
Sudan Kusini itakuwa nchi ya sita kujiunga na jumuiya hiyo iliyoanza kwa nchi tatu Tanzania, Kenya na Uganda. Rwanda na Burundi zilijiunga na jumuiya hiyo baadaye.
Sudan Kusini
Baada ya kujiunga rasmi leo, Sudan Kusini inatarajiwa kufungua mipaka yake kwa ajili ya biashara. Tayari kampuni na asasi nyingi za kifedha kutoka Kenya zimefungua vbiashara nchini Sudan Kusini.
Wengi wanatarajia hatua ya leo itafungua fursa zaidi za kibiashara kati ya Sudan Kusini na nchi wanachama wa jumuiya.
Wadadisi wengine wanaamini kuwa baadhi ya miradi ambayo Sudan Kusini ingetaka kujumuishwa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ni miundo msingi ikiwemo reli na mabomba ya mafuta.

Related Posts:

  • The Effects Of Negative Emotions On Our Health Humans experience an array of emotions, anything from happiness, to sadness to extreme joy and depression. Each one of these emotions creates a different feeling within the body. After all, our body releases different che… Read More
  • Familia ya dinosaria yapatikana TanzaniaMojawapo ya jamii wa awali wa dinosaria alikuwa na maumbile yanayofananishwa na mamba, matokeo ya utafiti Tanzania yanaonyesha. Wataalam wa masuala ya uhifadhi wa mabaki ya wanyama wamejiuliza familia ya dinosari wa kitambo w… Read More
  • Korea kaskazini: tupo tayari kwa vita kamili. Korea Kaskazini imeionya Marekani kutoanzisha vitendo vya uchokozi katika eneo la Korea ikisema kuwa iko tayari kulipiza kisasi kupitia mshambulio ya kinyuklia. Taifa hilo limesema hivyo wakati ambapo kiongozi wa Korea Kaskaz… Read More
  • What is 'Hyperinflation'What is 'Hyperinflation' Hyperinflation is extremely rapid or out of control inflation. There is no precise numerical indication of hyperinflation. Hyperinflation is a situation where the price increases are so out of control… Read More
  • Trump Aamuru Ndege za Kivita Zianze Kuruka Kuelekea Korea Kaskazini Ndege hatari na mpya zilizotengenezewa kwa teknolojia ya hali ya juu za F-35 Stealth Fighter Jets tayari zimeruka kutoka jimbo la Utah lililopo magharibi mwa nchi ya Marekani na kutua UK tayari kabisa kwa training ya mwisho … Read More