Recent Posts

PropellerAds

Wednesday, April 20, 2016

Mahakama yatupa 'sheria ya matusi' mtandaoni Kenya

Katiba
Mahakama Kuu jijini Nairobi imeamua kwamba Kifungu cha Sheria ambacho kimekuwa kikitumiwa kuwafungulia mashtaka watu kuhusiana na ujumbe kwenye simu na mitandao ya kijamii Kenya ni haramu.
Jaji wa Mumbi Ngugi alisema kifungu hicho, cha kutumia vibaya kifaa cha mawasiliano, kinakiuka katiba.
Kifungu hicho nambari 29 katika Sheria ya Habari na Mawasiliano Kenya Nambari 3 ya 1998 hupendekeza faini ya Sh50,000 au kifungo cha miezi mitatu jela, au adhabu zote mbili, kwa mtu anayepatikana na hatia.
Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) na Mwanasheria Mkuu walikuwa wametetea sheria hiyo wakisema ililenga kulinda sifa za wengine.
Jaji Ngugi alisema maelezo ya kifungu hicho ni mapana sana na pia baadhi ya makosa yanayolengwa kwenye kifungu hicho yameangaziwa katika sheria nyingine.
Aidha, alisema hakijatimiza matakwa ya Kipengele 24 cha Sheria ambacho kinaeleza ni katika hali gani ambapo haki za kimsingi zinaweza kubanwa. Aidha, alisema kifungu hicho kinakiuka Kipengele nambari 33 cha Katiba.
“Iwapo lengo ni kulinda sifa za watu wengine, basi hilo limeangaziwa kwenye sheria ya kuwaharibia sifa watu wengine,” Jaji Ngugi alisema kwenye uamuzi wake.
Jaji huyo alitaja mfano wa kesi tofauti dhidi ya mwanablogu mmoja ambaye aliamriwa kulipa Sh5 milioni na mahakama baada ya kushtakiwa chini ya sheria za kuwaharibia watu sifa.
Jaji Ngugi alikuwa akitoa uamuzi katika ombi la mwanablogu Geoffrey Andare aliyekamatwa Aprili 2015 na kufunguliwa mashtaka ya kutumia vibaya kifaa cha mawasiliano kutokana na ujumbe alioandika kwenye mitandao ya kijamii.
Mlalamishi alipinga mashtaka hayo akisema sheria hiyo inabana uhuru wa kujieleza mtandaoni.
Jaji alisema DPP hawezi kuendelea na kesi hiyo kwa msingi wa sheria hiyo.
Wakenya mtandaoni wamefurahia hatua hiyo ya Jaji Ngugi na tangu jana jioni jina lake limekuwa likivuma kwenye Twitter.
Kuna wanaomsifu kwa kutetea uhuru wa wananchi kujieleza lakini wengine wanahisi kwamba amekuwa akiharamisha vifungu vingi sana vya sheria.
Mfano ni Stephen Wambua anayesema uamuzi wa jaji huyo unafaa kuwekwa kwenye kitabu cha rekodi za dunia cha Guiness Book of World Records.
Mahakama Kuu jijini Nairobi imeamua kwamba Kifungu cha Sheria ambacho kimekuwa kikitumiwa kuwafungulia mashtaka watu kuhusiana na ujumbe kwenye simu na mitandao ya kijamii Kenya ni haramu.
Jaji wa Mumbi Ngugi alisema kifungu hicho, cha kutumia vibaya kifaa cha mawasiliano, kinakiuka katiba.
Kifungu hicho nambari 29 katika Sheria ya Habari na Mawasiliano Kenya Nambari 3 ya 1998 hupendekeza faini ya Sh50,000 au kifungo cha miezi mitatu jela, au adhabu zote mbili, kwa mtu anayepatikana na hatia.
Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) na Mwanasheria Mkuu walikuwa wametetea sheria hiyo wakisema ililenga kulinda sifa za wengine.
Jaji Ngugi alisema maelezo ya kifungu hicho ni mapana sana na pia baadhi ya makosa yanayolengwa kwenye kifungu hicho yameangaziwa katika sheria nyingine.
Aidha, alisema hakijatimiza matakwa ya Kipengele 24 cha Sheria ambacho kinaeleza ni katika hali gani ambapo haki za kimsingi zinaweza kubanwa. Aidha, alisema kifungu hicho kinakiuka Kipengele nambari 33 cha Katiba.
“Iwapo lengo ni kulinda sifa za watu wengine, basi hilo limeangaziwa kwenye sheria ya kuwaharibia sifa watu wengine,” Jaji Ngugi alisema kwenye uamuzi wake.
Jaji huyo alitaja mfano wa kesi tofauti dhidi ya mwanablogu mmoja ambaye aliamriwa kulipa Sh5 milioni na mahakama baada ya kushtakiwa chini ya sheria za kuwaharibia watu sifa.
Jaji Ngugi alikuwa akitoa uamuzi katika ombi la mwanablogu Geoffrey Andare aliyekamatwa Aprili 2015 na kufunguliwa mashtaka ya kutumia vibaya kifaa cha mawasiliano kutokana na ujumbe alioandika kwenye mitandao ya kijamii.
Mlalamishi alipinga mashtaka hayo akisema sheria hiyo inabana uhuru wa kujieleza mtandaoni.
Jaji alisema DPP hawezi kuendelea na kesi hiyo kwa msingi wa sheria hiyo.
Wakenya mtandaoni wamefurahia hatua hiyo ya Jaji Ngugi na tangu jana jioni jina lake limekuwa likivuma kwenye Twitter.
Kuna wanaomsifu kwa kutetea uhuru wa wananchi kujieleza lakini wengine wanahisi kwamba amekuwa akiharamisha vifungu vingi sana vya sheria.
Mfano ni Stephen Wambua anayesema uamuzi wa jaji huyo unafaa kuwekwa kwenye kitabu cha rekodi za dunia cha Guiness Book of World Records.




Related Posts:

  • Battling Sexual Sin The Evil Inside Me It's not surprising to me at all that given the sexual obsession of our culture and the pleasure-orientation of sin that somebody would struggle with lust. I can't blame my environment because it's alway… Read More
  • Loving the Unlovely Love That Makes the Beloved Beautiful Owing Beauty to God God’s love is different from human love because it is a beautifying love. God does not find people who are beautiful and then decide to love them. Rather, he make… Read More
  • 10 Things You Should Know about the Presence of God The mountains melt like wax at the presence of the LORD, at the presence of the Lord of the whole earth. Psalm 97: 5 1. God is immanent because he is transcendent. The Lord is “God in the heavens above (tr… Read More
  • 10 Things You Should Know about Suffering “Pain: the Gift Nobody Wants” 1. Suffering is a result of the fall. God warned Adam that eating the forbidden fruit would result in death (Gen 2). Romans 5:12 confirms that this happened after Adam’s fall, “Just as sin c… Read More
  • Your Last First Date It was our first date. I wasn’t even completely sure she knew it was a date. We met at a wedding, and then talked on the phone once a week or so for a couple of months. I asked if I could take her out, and she conceded. I b… Read More