Ibada maalum imeendelea leo huko Korea Kusini
kuadhimisha miaka miwili ya kuwapoteza watu mia tatu
wa taifa hilo ambapo wengi kati ya hao wana funzi,
ambao walikufa kutokana maafa kivukoni.
Ndugu waliokuwa wakiomboleza walionekana wakirusha
maua baharini karibu na mahali ambapo kivuko cha
Sewol kilipunduka.
Kikosi cha uokozi kinajiandaa kukiibua kivuko hicho ili
kuweza kupata miili ya watu wengine tisa ambao bado
hawajapatikana. Wakati kivuko hicho
kikizama,inasemekana kilikuwa kimebeba uzito uliozidi
uwezo wake kisheria.
Nahodha wa kivuko hicho tayari anatumikai kifungo cha
maisha gerezani kwa kosa la mauaji kizembe.
CCM wilaya ya mbogwe walia na tozo mazao ya chakula kwa wakulima.
-
Wananchi na Wakulima katika Halmashauri ya wilaya ya Mbogwe Mkoani Geita
wamewalalamikia viongozi wao wa kata kwa kushindwa kudhibiti Baadhi ya
watumishi...
1 hour ago