Recent Posts

PropellerAds

Sunday, April 3, 2016

Ndege yagonga gari California

Mtu mmoja ameuawa baada ya ndege moja kuangukia
gari alimokuwa kwenye barabara kuu ya California
Marekani.
Walioshuhudia wanasema kuwa ndege hiyo ilionekana
kama iliyokuwa na matatizo ya injini na ikalazimika
kutua kwa dharura kwenye barabara ya Interstate 15
freeway California.
Rubani wa ndege hiyo Dennis Hogge hata hivyo
alishindwa kuidhibiti na ikateleza na kuigonga gari
lililokuwa na abiria wanne lililokuwa limeegeshwa kando
ya barabara hiyo ilidereva azungumze kwa simu.
Mmoja aliaga dunia papo hapo huku wengine watatu
wakikimbizwa hospitalini katika hali mahututi.
Antoinette Isbelle, 38, kutoka San Diego alikuwa
ameketi nyuma katika gari hilo lililogongwa.
Yamkini hii sio mara ya kwanza kwa ndege hiyo kutua
kwenye barabra hiyo ya San Diego.
Mwaka wa 2000 mmiliki wa kwanza wa ndege hiyo
vilevile alipatwa na hitilafu ya kimitambo na akalazimika
kutua ndege hiyo hiyo chapa Lancair IV, kwenye
barabara hiyo hiyo.
Hata hivyo wakati huo tukio hilo halikusababisha maafa
wala uharibifu wa ndege hiyo.

Related Posts:

  • FAIDA ZA UFUGAJI NYUKI FAIDA ZA UFUGAJI NYUKI : Watu wengi duniani hudhania kwamba faida ya nyuki ni uzalishaji wa asali tu, na si vinginevyo. Lakini karne za hivi karibuni jinsi binaadamu walivyoanza kujihusisha na tafiti za wadudu mbalimbali, wa… Read More
  • Nine Words for Every Marriage Someday my children will introduce me to the person they intend to marry. When they do, there are three sentences — nine simple words total — that I want to know they can say, in earnest, before they can have my blessing:&… Read More
  • What About Those Who Have Never Heard? Dear _____, You asked what happens to people who live far away from the gospel and have never heard about Jesus and die without faith in him. Here is what I think the Bible teaches. God always punishes people because of … Read More
  • certain requirements we must fulfill before God will listen to our prayers. We Must Belong to God. “There is one God and one mediator between God and man, the man Christ Jesus” (1Timothy 2:5). Because Jesus is the mediator between us and God, we must give Him our total allegiance. Before I yield… Read More
  • KILIMO BORA CHA KAROTI UTANGULIZI Karoti ni zao la mbogamboga ambalo ni zao mzizi, kwa kawaida hupatikana katika rangi ya machungwa, zambarau, nyeusi, nyekundu, nyeupe na njano. Karoti za sasa zimetokeza kutokana na karoti pori, Daucus carota. K… Read More