Recent Posts

PropellerAds

Thursday, June 9, 2016

Kwanini ndoa za sasa hazidumu ?

Imezoeleka kwamba ndoa za kikatoliki zikifungwa zimefungwa pamoja na sharti hilo ,viwango vya ndoa zinazovunjika zinaendelea kuongezeka na kufuatia hali hiyo,kanisa katoliki limeamua kuanzisha tuzo maalumu kwa wandoa wakongwe zaidi kwa mwaka huu katika kanisa hilo.
Kanisa Katoliki jimbo kuu la Dar es salaam wameandaa kliniki ya ndoa ili kuweza kuwapa fursa wanandoa kuimarisha ndoa zao kiimani,Padre Novatus Mbaula ambaye ni mkurugenzi wa ndoa na familia anaeleza lengo la kliniki hii ni kuwapa nafasi wanandoa wa katika makundi mbalimbali kukaa pamoja kupata neno la Mungu na kuweza kuongea juu changamoto zao mbalimbali kuongea kuhusu maisha yao ya ndoa.
Ni nafasi ambayo wanandoa ambao wana uzoefu mkubwa katika ndoa wanaweza kuwafaidisha wanandoa wachanga lakini pia changamoto katika ulimwengu wetu wa sasa changamoto bado ni zilezile.
 

Miongoni mwa watu waliohudhuria kliniki hii ni wanandoa wenye ndoa yenye miaka 61,brigedia Generali mstaafu Francis Mbena,mwenye umri a miaka 86 alifunga ndoa akiwa na miaka 25 ,mwaka 1965 Juni,anasema wao zamani walikua wanafuata mtu na familia gani na ina vigezo gani?
Walikua wanaangalia tabia kama msichana hana tabia nzuri huoi huko; kama familia ina watu walevi uwaendei na unatafuta familia yenye watoto wenye tabia nzuri ili na wewe uweze kupata watoto wenye tabia nzuri.
Wakati mke wake ambaye ni Maura Stephen Mbena ambaye anasema asili yake ni Nyoni,yeye anasema ukiweza kumvumilia mwezako na ukamsamehe basi unaishi tu maana kukwaruzana kupo hakuishi na kikubwa ni kuvumilia.
Na katika mila na desturi za kabila yake ya wangoni, msichana kabla hajaolewa anaanapewa maneno na wazee ambao wazazi wako wamewaamini wanakupa msafara wote wa maisha ya ndoa,kwamba unapokwenda kuna matatizo pengine wakwe zao hawatakupenda au hautafanya vizuri kule na wanakupa muelekeo wa maisha ukavumilie na ukafanye hivi hivi lakini kikubwa sana ni sala.
Ndoa ni maisha yenye tafsiri nyingi,Bwana na bi.Alphonce Hurick walioko kwenye kipindi cha mwaka mmoja wa ndoa,wao wanaona maisha ya ndoa ni maisha yenye furaha,amani na upendo na ni maisha tofauti kabisa wakati kila mmoja akiishi peke yake peke yake,kwani hata kama una msongo wa mawazo kama ndoa yako ina furaha basi hayo matatizo yanakuwa hayapo kama ndoa yako ina upendo.
Bi.Kigadie ambaye yuko kwenye ndoa kwa miaka 46 na miezi mitano anaeleza jinsi walivyoingia kwenye ndoa na jinsi vijana wanavyoingia kwenye ndoa katika miaka ya sasa.
Anasema wengi hawakupata mafunzo ya kujua uchumba ni nini maana mapema mno wanageuza uchumba kuwa mme na mke kabla hawajapata sakramenti ya ndoa,sasa hilo ni tatizo ambalo wanajikuta wamepata ujauzito sasa ndoa inakuwa ya shuruti unaweza kuwa hata bwana alikuwa hana nia ya ndoa zaidi ya tamaa za kimwili na kimaisha.