Recent Posts

PropellerAds

Thursday, June 2, 2016

Dawa zilimuua Prince:Madaktari

Uchunguzi wa kidaktari kutoka jimbo la Minnesota nchini Marekani umebaini kuwa mwanamuziki Prince alikufa kutokana na kuzidisha kiwango cha dawa.
Kwa mujibu wa madaktari waliofanya uchunguzi huo wa kifo cha mwanamuziki Prince, wanasema alizidisha kiwango cha dawa za kutuliza maumivu zijulikanazokama Fentanyl .
Dawa hizo zinadaiwa kuwa na nguvu mara hamsini zaidi ya dawa za kulevya za Heroin.
Hata hivyo dawa hizo hutumika wakati wa upasuaji na hasa wagonjwa ambao miili yao ni sugu kwa dawa nyingine za kutuliza maumivu.
Prince alikutwa amefariki dunia mwezi april mwaka huu, ndani ya lift katika makazi yake huko karibu na mji wa Minneapolis .
Siku moja kabla ya kifo chake inadaiwa kuwa alikuwa akihitaji msaada kutokakwa daktari maalumu kutokana na maumivu aliyokuwa akiyasikia.
Polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi kutokana na kifo cha Prince