Afrika inatambuliwa kama mzalishaji muhimu wa mafuta na madini yanayohitajika na sekta ya kiviwada inayopanuka nchini India.
India pia ina lengo la kuboresha uhusiano ambao tayari umejengwa kati ya China na nchi za Afrika.
Afisa mmoja nchini India alizitaja nchi hizo tatu ambazo rais wa India atazizuru, kama zilizo na demokrasia iliyokomaa na dhabiti.