Recent Posts

PropellerAds

Thursday, June 16, 2016

Japan: Wanawake kuhifadhi mayai ya uzazi


Mamlaka ya mji mmoja nchini Japan, imeanza harakati ya kuwasaidia wanawake kugharimia malipo ya kuhifadhi mayai yao ya uzazi- kama hatua moja ya kujaribu kuimarisha viwango vya uzazi nchini humo.
Mji wa Urayasu, viunga vya jiji kuu Tokyo, umetenga dola laki nane u nusu kwa majaribio hayo ya kuhifadhi mayai ya uzazi, inayoaminika kuwa mradi wa kwanza kabisa wa aina yake duniani.
Wanasayansi katika hospitali iliyokabidhiwa majukumu hayo, wanasema kwamba, wanaimani kuwa uhifadhi ya mayai hayo ya uzazi itawasaidia wanawake kujifungua watoto wakiwa wamejiandaa ipasavyo, na kuongeza muda ambao watakuwa na watoto wao.
Serikali ya Japan inatafuta mbinu ya kuongeza idadi ya watu baada ya takwimu ya hesabu ya watu kubaini kuwa idadi ya raia nchini humo imeshuka kwa zaidi ya watu milioni moja katika kipindi cha miaka 5 tu iliyopita.