kundi la wanamgambo nchini Somalia,
al-Shabab, wanasema wamewaua watu watatu kwa kuwapiga risasi na
kumchinja shingo mwingine, baada ya kupatikana na hatia ya kuwa majasusi
wa mashirika ya ujasusi ya Kenya na Marekani.
Mauaji hayo yalitekelezwa mbele ya umati wa watu katika mkoa wa Bakool.
Kulingana na taarifa ya radio ya al-Shabaab,
mwanamume mmoja aliyeuawa ni Mohamed Aden Nur, ambaye anashutumiwa kuwa
aliwasaidia Wamarekani kumuua kiongozi wa kundi hilo Ahmed Godane.
Mwingine
aliyepigwa risasi anadaiwa kuwa alisaidia Wamarekani kumuua Adnan
Garaar, anayeaminika kuongoza shambulio la kigaidi katika duka la
Westgate nchini Kenya mwaka wa 2013
RC MALIMA ATAKA WANANCHI KUPIMA AFYA WAKATI WA KAMBI YA MADAKTARI BINGWA
-
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewataka wananchi wa
Mkoa huo kujitokeza kwa wingi kushiriki kupima Afya zao wakati wa Kambi
Maalum ya...
5 hours ago