Recent Posts

PropellerAds

Saturday, June 11, 2016

Al-Shabab ladai kuwaua wapelelezi wa Kenya na US

kundi la wanamgambo nchini Somalia, al-Shabab, wanasema wamewaua watu watatu kwa kuwapiga risasi na kumchinja shingo mwingine, baada ya kupatikana na hatia ya kuwa majasusi wa mashirika ya ujasusi ya Kenya na Marekani.
Mauaji hayo yalitekelezwa mbele ya umati wa watu katika mkoa wa Bakool.

Kulingana na taarifa ya radio ya al-Shabaab, mwanamume mmoja aliyeuawa ni Mohamed Aden Nur, ambaye anashutumiwa kuwa aliwasaidia Wamarekani kumuua kiongozi wa kundi hilo Ahmed Godane.
Mwingine aliyepigwa risasi anadaiwa kuwa alisaidia Wamarekani kumuua Adnan Garaar, anayeaminika kuongoza shambulio la kigaidi katika duka la Westgate nchini Kenya mwaka wa 2013