Recent Posts

PropellerAds

Sunday, June 12, 2016

Wakamatwa kwa kuwaingiza wanawake kwenye ukahaba


Polisi nchini Uhispania wametoa taarifa kuhusu oparesheni ya kimataifa, dhidi ya mtandao unaohusu kuwasafirisha wanawake kiharamu kwenda kufanya ukahaba ambapo watu 14 walikamatwa na wanawake saba kuokolewa.
Wanawake hao walikuwa ni kutoka nchini Paraguay. Watu wengi walikamatwa katika mji ulio kusini mwa Uhispania wa Pamplona.
Polisi walisema kuwa viongozi wa mtandao huo nchini Paraguay, walikuwa wamewaahidi wanawake hao ajira barani Ulaya, lakini badala yake wakawalazimisha kufanya ukahaba ili kulipa gharama yao ya usafiri.