Israel na Uturuki wanatarajiwa leo kutia sahihi
mapatano yanayonuia kumaliza uhasama kati ya
mataifa hayo mawili.
Uhusiano wa karibu baina ya mataifa hayo uliharibika
miaka sita iliyopita wakati wanamaji wa Israeli
waliposhambulia meli ya Wanaharakati wa Uturuki
waliokuwa wakipeleka msaada wa vyakula na madawa
huko Palestina kwenye ukingo wa Gaza na kuwaua 10
kati yao.
Maafisa kutoka mataifa hayo mawili wanasema kuwa
mapatano yameafikiwa kumaliza uhasama huo.
Uhusiano umeimarika tangu Waziri Mkuu wa Israil,
Benjamin Netanyahu na mwenzake wa Uturuki Recep
Tayyip kuwasiliana kwa simu mwaka wa 2013, kabla ya
mashauriano kuanza na yameimarika kwa miezi
michache iliyopita.
Miongoni mwa hatua za kwanza itakuwa kuwarudisha
mabalozi wa mataifa hayo waliorejeshwa nyumbani
baada ya meli ya wakereketwa wa Uturuki waliokuwa
wakisafirisha chakula kuwapelekea Wapalestina
kushambuliwa na Israel.
Aidha baadhi ya mapendekezo ni Israeli kuomba
msamaha kwa uturuki na kisha kufidia wanaharakati
waliouawa.
RC MALIMA ATAKA WANANCHI KUPIMA AFYA WAKATI WA KAMBI YA MADAKTARI BINGWA
-
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewataka wananchi wa
Mkoa huo kujitokeza kwa wingi kushiriki kupima Afya zao wakati wa Kambi
Maalum ya...
8 hours ago