Recent Posts

PropellerAds

Wednesday, June 22, 2016

Mji wa Hong Kong ndio ghali zaidi duniani


Mji wa Hong Kong ndio mji ghali zaidi duniani baada ya kuupiku mji wa Luanda, Angola kulingana na wafanyakazi wa kimataifa katika utafiti wa kila mwaka unaofanywa na shirika la Mercer.
Luanda ambao ulikuwa unaongoza orodha hiyo katika siku za hivi karibuni ulishuka kufuatia kudhoofika kwa sarufi yake.

Mji wa Zurich na Singapore ni ya tatu na nne mtawalia katika orodha hiyo ikiwa haijabadilika kwa mwaka mmoja sasa.
Mji wa Tokyo sasa umepanda hadi nafasi ya tano.
Utafiti huo unalenga kampuni zinazotakiwa kuhesabu marupurupu ya wafanyikazi wa kimataifa.
Umepima gharama ya kuishi kwa takriban mataifa 209 duniani,ikilinganisha gharama ya viti 200 katika kila eneo ikiwemo,bei ya nyumba ya kuishi,uchukuzi,chakula na burudani.