Recent Posts

PropellerAds

Monday, June 20, 2016

Al shabaab waua polisi 5 Mandera Kenya


Maafisa 5 wa polisi wa Kenya wameuawa mapema leo mjini Mandera katika shambulizi lililotekelezwa na wapiganaji wa kundi la wanamgambo la Al shabab kutoka Somalia.
Kamishna wa jimbo hilo la kaskazini mashariki mwa Kenya bwana Job Borongo ameithibitishia BBC kuwa wapiganaji hao walifanya shambulizi la kuvizia dhidi ya msafara wa magari ya polisi uliokuwa ukienda El Wak wakitumia guruneti.
Maafisa hao tano waliangamia papo hapo huku gari walimokuwa wakisafiria likiharibiwa kabisa.
Maafisa wengine wanne wamejeruhiwa vibaya.
Msafara huo wa polisi ulikuwa ukitoa ulinzi kwa msafara wa mabasi ya uchukuzi wa umma, desturi iliyoanzishwa baada ya wapiganaji hao kuteka basi moja na kuua abiria 28 wakristu.
Gavana wa Mandera bwana Ali Roba aliwalaumu maafisa wa polisi katika eneo hilo kwa kupuuza tahadhari iliyotolewa na wenyeji kuhusiana na mashambulio ya kigaidi.

Roba anasema walipuuza vyanzo vya kiintelijensia vilivyotolewa kuhusiana na kuonekana kwa wapiganaji hao waliojihami.
Hii si mara ya kwanza Mandera kushuhudia mashambulizi ya al shabaab.
Shambulizi hilo la Novemba mwaka wa 2014 liliwaacha wasafiri wengi wasiokuwa waislamu na hofu ya kusafiri na hivyo kuilazimu serikali kutoa usalama kwa mabasi ya uchukuzi wa umma.
Mwezi mmoja baadaye wapiganaji hao waliwaua wachimba migodi 36 katika eneo hilo la Mandera.
Kundi hilo la wapiganaji wa kiislamu limekuwa likitekeleza mashambulizi katika maeneo ya kaskazini mwa Kenya likitaka kuishinikiza taifa hilo jirani kuondoa majeshi yake nchini Somalia.

Image caption Gavana wa Mandera bwana Ali Roba aliwalaumu maafisa wa polisi katika eneo hilo kwa kupuuza tahadhari iliyotolewa na wenyeji
Kenya ilipeleka vikosi vyake vya jeshi nchini Somalia mwaka wa 2011 ikitaka kuzima mashambulizi ya mara kwa mara.
Hata hivyo kundi hilo limeongeza mashambulizi nchini kenya ikiwemo mauaji ya watu 67 katika maduka ya Westgate mjini Nairobi mwaka wa 2013.
Mwaka uliopita Al Shabab ilitekeleza mashambulizi katika chuo kikuu cha Garissa na kusababisha vifo vya wanafunzi 148

Related Posts:

  • The Three Breeds of Gossip "A man of knowledge uses words with restraint, and a man of understanding is even-tempered.  Even a fool is thought wise if he keeps silent, and discerning if he holds his tongue' without wood a fire goes out;… Read More
  • I AM NOT Ashamed of the Gospel Truth Taught- Paul is obligated, eager and not ashamed to preach the Gospel because it is God’s power to salvation for all who believe. Introduction Our text today shows us Paul’s responsibility and passion to preach and … Read More
  • Don’t Give Up “Here is a call for the endurance of the saints” (Revelation 14:12). We all long for rest from the fatigue of living. God placed the desire for rest in our souls, and he promises to fulfill it: “I will satisfy the weary s… Read More
  • Helping Each Other Endure to the End Fifty years ago evangelicals in Germany formed what became known as the Confessing Church. They opposed the German Christian Church Movement sponsored by the Nazis between 1933 and 1945. As Nazi dominance increased, the Co… Read More
  • Lord, Set Me Free from Fear On Thursday night, Peter said to the One he knew was “the Christ, the Son of the living God” (Matthew 16:16), “Even if I must die with you, I will not deny you!” (Matthew 26:35). Then, in the wee hours of Friday morning,… Read More