Recent Posts

PropellerAds

Thursday, March 31, 2016

MAGAZETI YA LEO TZ,APRIL MOSI

...

Wafadhili wasitisha ufadhili kwa bajeti ya Tanzania

Mataifa 10 ya Magharibi yamesema hayataendelea na ufadhili wao kwa bajeti ya serikali ya Tanzania. Baadhi ya nchi hizo ni Sweden na Ireland. Nchi hizo zinaendelea na msimamo huo ikiwa ni siku chache baada ya shirika la utoaji misaada la serikali ya marekani (MCC) kuondoa msaada wake wa dola 472 za ufadhili wa miradi ya maendeleo kwa Tanzania. Bodi ya MCC ilisema hatua yake...

Aliyewakinga wakristo kutoka kwa al shabab atuzwa

Marehemu mwalimu aliyepigwa risasi akiwakinga wakristo wasiuawe na magaidi wa Al Shabab ametuzwa medali ya juu zaidi na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta Rais Kenyatta alipokuwa akihutubia taifa alisema kuwa wale wakenya wachache wanaoonesha ujasiri wa kukabiliana dhidi ya al shabab watatuzwa. Rais Kenyatta alihutubia taifa Na hivyo akasema kuwa Mwalimu Farah ametuzwa heshima ya...

Mwana wa Besigye awania urais Oxford

Mwana wa kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kizza Besigye ni miongoni mwa wanafunzi waliojitokeza kuwania urais katika chama cha mijadala chuo cha Oxford. Anselm Besigye ametengeneza video fupi ya kuwaomba wanafunzi wenzake wampigie kura. Anasimulia mambo ambayo amefanyia chama hicho na uzoefu wake katika mijadala. Mwisho wa video mamake Anselam Winnie Besigye, anaonekana...

Waziri wa Rwanda afia gerezani Burundi

Waziri wa zamani wa Rwanda Jacques Bihozagara amefariki katika gereza moja nchini Burundi miezi minne baada ya kukamatwa kwa tuhuma za kufanya ujasusi. Rwanda imesema marehemu Jacques alikuwa ameshikiliwa kinyume cha sheria. Balozi wa Rwanda nchini Ubelgiji ameandika na kusema kifo cha Jacques ni "mauaji". Wafungwa katika gereza alipokuwa ameshikiliwa wanasema alionekana akiwa...

Wafadhili wasitisha misaada kwa Tanzania

Kundi la watoa misaada 10 kutoka nchi za magharibi wametangaza kusitisha ufadhili wao kwa bajeti ya serikali ya Tanzania. Hii inafuatia uamuzi wa shirika la utoaji misaada la serikali ya marekani kuondoa msaada wa dola 472 wa kufadhili miradi ya maendeleo kutokana na jinsi uchaguzi wa kisiwa cha Zanzibar ulivyoendeshwa. Karibu theluthi moja ya bajeti ya Tanzania ilitegemea msaada...

Daraja laporomoka na kuwaua 10 India

Takriban watu 10 wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya daraja moja la juu lililokuwa likijengwa kuporomoka kwenye mji wa mashariki mwa India wa Kolkata Ripoti zingine zinasema kuwa karibu watu 150 huenda wamekwama chini ya vifusi vya daraja hilo lililo eneo lenye shughuli nyingi. Miradi ya ujenzi nchini India mara nyingi imekumbwa na matatizo ya kiusalama na huporomoka...

Chama chatisha kumuondoa Zuma madarakani

Chama cha Democtratic Alliance nchini Afrika Kusini kumeanzisha kampeni ya kumuondoa rais Jacob Zuma madarakani baada ya mahakama ya kikatiba kutoa uamuzi kuwa alikiuka katiba. Mahakama ilipata kuwa bwana Zuma alikataa kutii agizo kutoka kwa ofisi ya mwendesha mashtaka mkuu mwaka 2014 la kamtaka alipe pesa zilizotumika kuifanyia ukarabati nyumba yake ya kibinafsi. Vyama viwili...

Trump ayumbayumba kuhusu utoaji mimba

Mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump amebadili msimamo wake muda mfupi baada ya kusema wanawake wanaotoa mimba wanafaa kuadhibiwa, utoaji mimba ukiharamishwa. Alikuwa ametoa tamko lake katika hafla iliyopeperushwa moja kwa moja na kituo cha runinga cha MSNBC. Hatua hiyo ilimfanya kushutumiwa vikali. Lakini muda muda mfupi baadaye, alibadili msimamo wake...

Wednesday, March 30, 2016

HOTUBA YA TRUMP YATUMIKA KATIKA FILAMU

Wazalishaji wa filamu moja nchini Mexico kuhusu wahamiaji wanaojaribu kuingia nchini Marekani wametoa kipande kidogo cha filamu hiyo ambacho kinatumia hotuba ya bwana Donald Trump kupitisha ujumbe wa filamu hiyo kwamba maneno ni hatari kama risasi. Sauti iliowekwa katika filamu hiyo ya Kihispania, Desierto ,inemuonyesha bwana Trump akiitaka Mexico kusitisha kuwaingiza Marekani...

MAGAZETI YA LEO MARCH 31

...

Ajali ya ndege yawaua watu 7 Canada

Watu saba wamefariki baada ya ndege moja ya kibinafsi kuanguka katika kisiwa cha mashariki ya pwani ya Quebec. Mamlaka imesema kuwa ndege hiyo ilianguka ilipokuwa ikikaribia uwanja wa ndege wa Madeleine huku kukiwa na upepo mkali pamoja na barafu. Jean Lapierre,aliyekuwa waziri wa uchukuzi nchini Canada pamoja na watu wa familia yake walikuwa miongoni mwa waathiriwa. Bwana...

Marekani yalalamikia UN kuhusu Iran

Marekani na washirika wake kutoka Ulaya wameulalamikia Umoja wa Mataifa kuhusu hatua ya Iran ya kufanyia majaribio makombora ya masafa marefu. Mataifa hayo yamesema majaribio hayo yanakiuka azimio la Umoja wa Mataifa. Azimio hilo ambalo liliidhinisha mkataba wa nyuklia baina ya UN na Iran liliitaka Iran kutofanyia majaribio makombora ya masafa marefu yenye uwezo wa kubeba silaha...

Monday, March 28, 2016

MAGAZETI YA LEO TZ,MARCH 29

...